Hili linafahamika na hata viongozi wetu wamekuwa wakisema kuwa Kiswahili ndiyo lugha yetu yaTaifa.
Binafsi siamini kama kauli hii ina ukweli ndani
yake kwa sababu Watanzania tumeshindwa kukienzi Kiswahili, licha ya kuwa
lugha hiyo ni ya 10 duniani kwa idadi ya wazungumzaji, inazungumzwa na
watu takriban 100 milioni.
Hivi karibuni Serikali ilieleza mkakati wake wa
kuhakikisha Kiswahili kinazungumzwa katika makongamano ya kitaifa na
kufundishia, lakini binafsi siamini kama juhudi hizo zitaweza kuifanya
lugha hiyo ilingane na hadhi yake ya kuwa moja ya lugha 10 duniani.
Serikali imetufumbua macho baada ya kueleza wazi
kuwa Kiswahili ni kati ya lugha 10 zinazozungumzwa zaidi duniani, lakini
wakati huohuo wanaofundisha Kiswahili katika vyuo vikuu nje ya nchi
siyo Watanzania, lakini kama hilo halitoshi hata viongozi wetu wakiwa
katika makongamano nao wanakikacha Kiswahili na kuzungumza Kiingereza
hivyo kuwaacha kwenye mataa Waswahili.
Zaidi ya asilimia 90 ya Watanzania wanazungumza Kiswahili, lakini hakuna juhudi za makusudi za kuimarisha lugha hii.
Huwa najiuliza maswali mengi ninapowasikia viongozi wetu wakisema kuwa Kiswahili ndiyo lugha ya taifa.
Kama jibu ni ndiyo, inakuwaje sekta nyeti za nchi
hii kama Mahakama, Serikali na taasisi nyingi wanatumia lugha ya
Kiingereza. Sijui matumizi haya ya Lugha ya Kiingereza yana lengo gani
katika nchi hii ya Waswahili inayoaminika kuwa ndiyo chimbuko la
Kiswahili duniani.
Sikatai, wapo wanaokitetea Kiingereza kwamba ni
lugha ya kibiashara duniani hivyo Watanzania ni lazima wajifunze na
kukijua kwa ufasaha.
Sasa kama ukweli ndiyo huo kuna ulazima gani kwa
Kiingereza kutumika mahakamani wakati idadi kubwa ya wanaokwenda
mahakamani ni Waswahili wasiokijua kwa ufasaha Kiingereza.
Hivi sasa taifa letu halijui lisimame wapi, na nathubutu kusema kwamba kuendekeza Kiingereza ndiyo chanzo cha idadi kubwa ya wanafunzi kushindwa kufanya vyema katika masomo yao, Wengi wao hivi sasa wanakariri tu maswali na majibu, ukiligeuza swali wanashindwa kulifanya kwa sababu ya kutojua Kiingereza. Mwanafunzi anaanza darasa la kwanza hadi la saba akifundishwa kwa kutumia lugha ya Kiswahili, anapoanza kidato cha kwanza anakutana na lugha ya Kiingereza.
Hivi sasa taifa letu halijui lisimame wapi, na nathubutu kusema kwamba kuendekeza Kiingereza ndiyo chanzo cha idadi kubwa ya wanafunzi kushindwa kufanya vyema katika masomo yao, Wengi wao hivi sasa wanakariri tu maswali na majibu, ukiligeuza swali wanashindwa kulifanya kwa sababu ya kutojua Kiingereza. Mwanafunzi anaanza darasa la kwanza hadi la saba akifundishwa kwa kutumia lugha ya Kiswahili, anapoanza kidato cha kwanza anakutana na lugha ya Kiingereza.
Kwa mantiki hiyo ni wazi kuwa hatafanya vyema
katika masomo yake, hasa kama hatakuwa na msingi mzuri katika lugha ya
Kiingereza.
Kiswahili kikipewa kipaumbele taifa litapiga hatua kubwa kimaendeleo katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu.
Nasema hivyo kwa sababu maarifa na lugha ni vitu
viwili tofauti. Hivyo mtu anapofundishwa somo la Jiografia, Historia,
Fizikia kwa Kiswahili ataelewa zaidi na atapata maarifa
yatakayomwezesha kunufaika yeye na jamii inayomzunguka.
Source Mwananchi
Source Mwananchi
No comments:
Post a Comment