Saturday, July 16, 2016

Prof Muhongo ahimiza kilimo cha Alzeti katika jimbo la Musoma vijijini

               Mkulima wa zao la Alzeti akitazama zao hilo shambani
                         Baadhi ya wakulima hao wakifanya Mahojiano na AZAM TV
      Afisa kilimo kata ya Nyakatende Bw Magesa akisema zao hilo ni mbadala wa Pamba

Kusuasua kwa kilimo cha Pamba na kushambuliwa na Magonjwa kwa zao la Muhogo katika Halmashauri ya Musoma vijijini wilaya ya Musoma mkoani Mara mazao ambayo yalikuwa ya chakula na Biashara kumesababisha viongozi katika halmashauri hiyo kuanzisha kilimo cha Alzeti,Zao ambalo linaelezwa linaweza kuwa mbadala wa Mazao hayo.

Kwa muda mrefu sasa wananchi wa halmashauri ya Musoma vijijini wilaya ya Musoma mkoani Mara wamekuwa wakihangaika katika kilimo cha Pamba kama zao la Biashara na Muhogo kama zao la Chakula lakini mabadiliko ya Tabia nchi na Magonjwa ya Michilizi kahawia na Batoto kwa zao la Muhogo yamekuwa kikwazo kikubwa.

Kufuatia hatua hiyo wananchi hao wamehimizwa kuanzisha kilimo za Alzeti kilimo ambacho kinaelezwa kinaweza kuwa mbadala wa Mazao hayo endapo wananchi hao watafuata kanuni za kilimo.

Hata hivyo licha ya wananchi hao kujikita katika kilimo cha Alzeti bado wanaiomba serikali kuwa karibu katika kuhakikisha kilimo hicho kinakuwa na Tija.

Afisa kilimo katika kata ya Nyakatende Halmashauri ya Musoma vijijin MAREGESI EPHRAIM akaomba Mbunge wa jimbo hilo na viongozi wa halmashauri hiyo kuhakikisha vinapatikana viwanda vidogo vitakavyosaidia wananchi hao baada ya kuvuna Alzeti hiyo.

Mbunge wa Jimbo la Musoma vijiji Mbunge wa jimbo hilo Prof Sopeter Muhongo ambaye pia ni waziri wa Nishati na Madini amesema Alzeti ni zao pekee ambalo litakuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa jimbo hilo kufuatia kushuka kwa soko la Pamba na zao la Muhogo kushambuliwa na Magonjwa mbalimbali.

KUTOKA MAKTABA YA MWANA WA AFRIKA



Tuesday, April 12, 2016

Makamu wa Rais Mh SAMIA SULUHU azindua kongamano la wanawake katika uongozi

c1Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Mhe. Zakia Meghji alipowasili ukumbi wa Mwalimu Nyerere kwa ajili ya kuzindua Kongamano la Wanawake katika Uongozi linalojadili kuendeleza Mazingira kuwezesha kuinua Wanawake ambao bado hawajapata fursa kufikia nafasi za Uongozi. Kongamano hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi limefanyika leo April 12, 2016.
C2Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizindua Kongamano la Wanawake katika Uongozi linalojadili kuendeleza Mazingira kuwezesha kuinua Wanawake ambao bado hawajapata fursa kufikia nafasi za Uongozi. Kongamano hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi limefanyika leo April 12, 2016 katika ukumbi wa Mwalim Nyerere.
C3Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati akiwa katika picha ya pamoja na Wanawake waliohudhuria Kongamano la Wanawake katika Uongozi linalojadili kuendeleza Mazingira kuwezesha kuinua Wanawake ambao bado hawajapata fursa kufikia nafasi za Uongozi. Kongamano hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi limefanyika leo April 12, 2016 katika ukumbi wa Mwalim Nyerere.
C4Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Waandishi wa Vyombo vya Habari baada ya kuzindua Kongamano la Wanawake katika Uongozi linalojadili kuendeleza Mazingira kuwezesha kuinua Wanawake ambao bado hawajapata fursa kufikia nafasi za Uongozi. Kongamano hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi limefanyika leo April 12, 2016 katika ukumbi wa Mwalim Nyerere.

Saturday, April 9, 2016

RC MULONGO atoa wiki mbili kwa Mkurugenzi H/Rorya kuhakikisha Kituo cha Afya Kinesi kinaanza kazi

                           Jengo la kituo cha Afya kinesi kwa nyuma
                           Baadhi ya wananchi wa kinesi wakiwa katika jengo la upasuaji la kituo cha Afya
                          Wananchi wakiendelea kumsikiliza RC Mulongo
                              Vifaa vilivyopo katika kituo hicho

Mkuu wa mkoa wa Mara Bw MAGESA MULONGO ametoa wiki mbili kwa 
Mkurugenzi wa halmshauria ya wilaya ya Rorya kuhakikisha kituo cha Afya cha Kinesi kinaanza kazi ya upasuaji.

Kauli ya mkuu huyo wa mkoa inafuatia kususua kuanza kutumika kwa jengo hilo kutokana na tatizo la kutokuwepo kwa huduma ya umeme na Maji hivyo kusababisha wananchi katika kijiji hicho kutafuta huduma za upasuaji katika hospital ya Rufaa ya mkoa wa Mara.

  " Mkurugenzi na mhe Makamu Mwenyekiti ndani ya wiki mbili nataka kituo hiki kiwe kimeanza kazi,mtajua mtakapotoa hela lakini ninachotaka ni hiki kituo kianze kazi ndani ya siku kumi na nne"alisema Bw Mulongo 

Tuesday, April 5, 2016

Zaidi ya watoto 20,000 kurejeshwa Shuleni-Mara

                        Mkuu wa mkoa wa Mara Bw MAGESA MULONGO kushoto

                             Bw Joshua mirumbe-Mkuu wa wilaya ya Bunda
                                              Baadhi ya wajumbe walioudhuria
                                Askofu Michael Msonganzila
                                                 Bi GRACA MACHAEL
                                                         RC Mulongo
                                          Wakili Ostack Mligo

Monday, April 4, 2016

MAGESA MULONGO atangaza vita kwa wanaomiliki silaha kinyume na utaratibu

                         Bw MAGESA MULONGO - RC MARA

Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw MAGESA MULONGO ametoa wiki tatu kwa wale wanaomiliki silaha kinyume na utaratibu kusalimisha silaha hizio haraka huku wanaomili ndani ya utaratibu kupeleka zikaguliwe.

RC Mulongo ametoa agizo hilo wilaya ya Bunda mkoani Mara baada ya kukutana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Mara ambapo alisema baada ya kukamilika wiki hizo oparesheni kali itafuata.

Wednesday, February 24, 2016

Wanahabri,Watafiti kutoka COSTECH wazuru kaburi la Baba wa Taifa Butiama mkoani Mara


Wanahabari na Watafiti kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), waliokuwa katika ziara ya kuzungumza na wakulima wa mkoa wa Mwanza kuhusu changamoto za kulimo zinazo wakabili pamoja na matumizi ya bioteknolojia katika kilimo wakiwa mbele ya kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere walipozuru kaburi hilo hivi karibuni Kijiji cha Mwitongo Butiama mkoani Mara.
Watafiti na wanahabari hao wakiwa mbele ya makaburi ya wazazi wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.
Mtafiti Kiongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknnolojia (Costech), Dk.Nicholaus Nyange (kushoto), na Mtafiti Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Dk.Emmarold Mneney wakiwa wamesimama ilipo sanamu ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Hapa ni picha ya pamoja katika sanamu ya Baba wa Taifa.
Mwendeshaji wa mtandao wa www. habari za jamii.com Dotto Mwaibale akivinjari katika moja ya jengo katika makazi ya Baba wa Taifa.
Matembezi yakiendelea katika makazi ya Baba wa Taifa.
Mratibu Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Afrika, Daniel Otunge (kushoto) Mtafiti Kiongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknnolojia (Costech), Dk.Nicholaus Nyange (katikati), na Mtafiti Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Dk.Emmarold Mneney wakiwa wamekaa katika kibanda alichokuwa akipenda kupumzika Hayati Nyerere wakati wa 
uhai wake.
Jamii inayofanya shughuli mbalimbali nyumbani kwa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere wakionesha upendo kwa kunywa chai pamoja katika makazi ya Mwalimu Nyerere yaliyopo Kijiji cha Mwitongo, wilayani  Butiama mkoani Mara kama walivyonaswa na kamera yetu katika ziara hiyo.
Picha ya pamoja katika nyumba maalumu lilipo kaburi na Mwalimu Nyerere.
Dereva wa Msafara huo, Mr Stanley akiwa mbele ya gari na mtafiti Kutoka Kituo cha Utafiti cha Ukiriguru cha jijini Mwanza, Isabela Msuya.
Mwendeshaji wa mtandao wa www. habari za jamii.com Dotto Mwaibale akiweka maua kwenye kaburi la Baba wa Taifa

Saturday, February 20, 2016

Wakulima Mara wapata Mafunzo ya kupashana habari za kilimo kwa njia ya simu


Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Philbert Nyinondi (kulia), akizungumza na wakulima na Washiriki wa Mafunzo ya kutumia simu za mkononi kupashana habari za kilimo yaliyofanyika Kijiji cha Kisamwene wilayani Butiama mkoani Mara leo mchana.
Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Philbert Nyinondi (kulia), akiwaonesha wakulima wa Wilaya ya Butiama mkoani Mara zao la mhogo uliotokana na mbegu aina ya ukombozi iliyofanyiwa utafiti nchini. Nyinondi alikuwa akiwaonesha wakulima jinsi unavyoweza kupiga picha zao hilo na kulitafutia soko wakati akitoa mafunzo ya kutumia simu jinsi kupashana habari za kilimo katika mafunzo yaliyofanyika juzi wilayani humo.
Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia za Kilimo Afrika (OFAB), Daniel Otunge akiwa katika shamba la mkulima wa mfano lililopo kijijini hapo.
Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia za Kilimo Afrika (OFAB), Daniel Otunge akimpiga picha mmoja wa wakulima katika mafunzo hayo.
Wakulima washiriki wa mafunzo hayo wakiwa ukumbini.
Wakulima wakiwa katika shamba la mihogo.
Mkulima akichimba muhogo wa mafunzo kutoka shamba hilo. Muhogo huo ni wa miezi nane tu.
 
Shamba la muhogo lililotokana na mbegu bora ya mkombozi.
Wakulima wakiwa katika mafunzo hayo.
Wakulima wakiwa katika mafunzo ya kupiga picha.
Wakulima wakiwa katika mafunzo ya kupiga picha.
Hapa wakulima hao wakibadilishana mawazo baada ya kupiga picha za mafunzo.
…………………………………………………………………………………………………..
Na Dotto Mwaibale

JUKWAA la Bioteknolojia (OFAB) limetoa mafunzo ya kutumia simu katika kupashana habari kwa wakulima wilayani Butiama mkoani Mara ili kuwarahisishia kazi zao za kilimo.
Akizungumza katika mafunzo hayo Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Philbert Nyinondi alisema mafunzo hayo ya siku moja yalifanyika katika Kijiji cha Kisamwene wilayani humo ili kuwasaidia wakulima kupashana habari za kilimo na changamoto zao.
“OFAB imeleta mafunzo haya kwa wakulima ambao ni wadau wetu ili waweze kupashana habari za kilimo, changamoto zinazo wakabili na kutafuta masoko ya mazao yao kwa njia ya simu badala ya kutumia simu hizo kupigiana kwa mambo ya kawaida” alisema Nyinondi.
Alisema kupitia mafunzo hayo wakulima hao wataweza kushirikiana na mitandao mingine ya kijamii ili kutatua changamoto zao za kilimo zikiwemo za wadudu waharibifu wa mazao, ukame na nyinginezo.
Alisema washiriki wa mafunzo hayo walikuwa ni 28 kutoka Kata tano zilizopo wilayani Butiama mkoani humo na yaliwahusisha viongozi wa vijiji, kata na wenyeviti wa serikali za mitaa.