Monday, September 17, 2012

MPWA WA GEORGE MARATO AKITIMIZA MOJA YA MILA ZA KIKURYA,PICHA 30 ZA TOHARA KATIKA KIJIJI CHA RYAMISANGA, PART 1

      *Picha 30 za sherehe ya Mpwa wake na  Mwandishi wa habari wa ITV & Redio one mkoani Mara George Marato,Mkazi wa kijiji cha Ryamisanga wilaya ya Butiama Mkoani Mara.Taarifa zinasema kuwa kwa mila ya Kabila ya Kikurya unapokaribia kutimiza Umri wa utu uzima lazima utairiwe na hivyo kuruhusiwa kuingia katika Mapenzi na kushiriki katika Tambiko zote za Kimila.

      *Lakini pamoja na kutimiza moja ya mila katika kabila hilo lakini pia wataalamu wa Afya wanasema kuwa mtu anapotairiwa ana zaidi ya asilimia 60 kujikinga na magonjwa Mbalimbali ukiwemo Ugonjwa wa Ukimwi,kufuatia hatua hiyo Serikali ya Tanzania iliamua kufanya zoezi hilo la kutairi baadhi ya Mikoa hapa Tanzania ukiwemo mkoa wa Mara katika wilya ya Rorya

   *   Matukio yote utayapata kupitia blog hii ya Mwana wa Afrika na hapa ni Part 1
Umati mkubwa wa watu wakicheza ngoma ya kikurya "Maarufu kama LITUNGU kabla ya tohara kufanyika
 Marato yupo kati akimwaga noti kwa kijana kwa kuonyesha ujasiri wa kukubali kutimiza mila ya kabila yao
               Noti bado zinaendeleee kumiminwa
                          Baada ya kutoa noti jamaa akaingia kati kucheza ngoma
                     Dogo bado anachemsha damu kwa kucheza ngoma  ya Kikurya
             Akina mama hawapo nyuma katika kusherekea sherehe hiyo
             Huyu jamaa anayepiga lilandi cjui akitoaka hapo Msosi utasalimika
        Kushoto Mwana wa Afrika kuli Shommy B tuliamua kumuunga Mkono Kijana
                                                  Noti zaendelea kumiminika


                                Shommy B akiwa ameshika kitu,cjui nininin?
  Maria Marato kushoto na Marato kulia wakiwa na ndugu yao ambaye jana ametimiza Moja ya Mila za Kikurya
    Hawa Jamaa waliishatimiza hiyo mila na hapa wanamtazama Mwenzao kama atalia au vp
   Marato kama vile aamini kama mdogo atavumilia kisu kukamilisha Moja ya mila ya Kabila lao
                       Jamaaa wana Mbwembwe hawaaaaaaaaaaaaa
     Dakika ya Mwisho kabisa kabla ya Kisu Marato akarudi tena na kuanza kutoa Msimbazi kibao


            Du  muda ukawadia, huyu jamaa anayevaa groves tayari kwa kumaliza kazi kwa kijana
                Tayari mambo yameiva na kijana kaishatoa bukta kama ni kufa nife
                        Jamaa akasogea  mbele ya Kijana tayari kwa kumaliza kazi
                   Haya sasa mambo ndyo hayo,jamaa kaanza kufanya Mambo

                Endelea kuangalia Blog hii uone nn kitafuatia je kijana alilia au vp?

No comments:

Post a Comment