Thursday, July 26, 2012

WAZIRI MKUU PINDA AONGOZA MAMIA YA WANA MUSOMA KUMUAGA MWALIMU ALIYEMFUNDISHA BABA WA TAIFA.MWALIMU JAMES IRENGE LEO

          Wadau wakitaza picha walizopiga
 Mwakilishi wa Vfm Mara akifanya mahojiano na mkuu wa wilaya ya Serengeti juu ya kifo cha Mwl James Irenge
   Ndege iliyombeba Waziri mkuu Pinda ikiwasili katika uwanja wa ndege wa Musoma leo Asubuhi
  Waziri mkuu akisalimiana na Viongozi baada ya kufika katika uwanja wa Ndege Musoma
Waziri mkuu Mizengo Pinda akitoa heshima za Mwisho kwenye Jeneza la hayati Mwl James Irenge leo mjini Musoma
 Mke wa Waziri mkuu Tunu Pinda akitoa heshima za Mwisho
Mbunge wa jimbo la Musoma mjini Mh Vincent Nyerere akitoa heshima za Mwisho kwenye Jeneza la hayati mwalimu James Irenge
     Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini  Mh Nimrodi Mkono akitoa heshima za Mwisho kwa Hayati Mwalimu James Irenge
 Aliyewahi kuwa mbinge wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo akitoa heshima kwenye jeneza la hayati Mwl James Irenge

Musoma'

 Waziri Mkuu Mizengo Pinda ameongoza Mamia ya Wananchi mkoani Mara kumuaga aliyekuwa Mwalimu wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage,Mzee James Irenge katika kijiji cha Busegwe wilayani Butiama mkoani Mara

 Akitoa salaam za rambirambi nyumbani kwa Marehemu James Irenge Musoma mkoani Mara,Waziri mkuu Pinda amesema kuwa Mzee Irenge mbali na kutofahamika sana lakini alikuwa ni mtu mwenye historia kubwa nchini kutokana na Mchnago wake wa kumlea Nyumbani kwake na kumfundisha darasani Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika shule ya Mwisenge mjini Musoma darasa la tatu na nne

Akisoma maombi maalum ya Familia ya Marehemu mzee James Irenge  kwa Waziri mkuu,mmoja wa wanafamilia Bw Arthur Irenge amemuomba waziri mkuu kusaidia Familia hiyo kupata kiinua Mgongo alichostahili kulipwa baada ya kustaafu kazi mwaka 1970.

Marehemu Mwalimu James Irenge alifariki dunia Julai 21 mwaka huu akiwa na Umri wa miaka 120,ameacha Mjane na watoto wanane

No comments:

Post a Comment