SMZ KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA USALAMA KWA WATALII
Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi Zanzibar
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imeahidi kukuza na kuimarisha
miundombinu ya kiusalama kwenye Sekta ya Utalii ili kuwafanya wageni
wanaitembelea Zanzibar kuwa salama wakati wote wanapokuwa hapa nchini.
Ahadi
hiyo imetangawa za Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Zanzibar Dk. Mwinyihaji
Makame Mwadini, wakati akifunga maunzo kwa Askari wa Kikosikazi cha
Doria ya Utalii yaliyokuwa yakiendeshwe kwenye Chuo cha Polisi cha
Zanzibar.
Mafunzo
hayo ya pamoja ya miezi miwili, yamewashirikisha Maafisa na Askari
kutoka Jeshi la Polisi, Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji (KZU, Kiukosi
Maalum cha Kuzuia Magendo (MKMK), Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU), Chuo
cha Mafunzo(Magereza), Kikosi cha Valantia (KVZ) pamoja na Maafisa wa
Kamisheni ya Utalii Zanzibar.
Waziri
Mwinyihaji amesema kuwa kuanzishwa kwa kikosikazi hicho kutasaidia kwa
kiasi kikubwa katika kulinda usalama wa watalii wanaoitembelea nchi na
watakapoondoka wataweza kuvuta wageni wengine na hivyo kuimarisha utalii
na kukuza pato la Taifa.
Amesema
kuwa kutokana na kwamba zaidi ya aslimia 70 ya wananchi wa Zanzibar
wameajiriwa na kunufaika na Sekta ya Utalii ambao pia unaliingizia taifa
zaidi ya aslimia 80 ya pato la uchumi, Serikali ya Zanzibar imeazimia
kuhakikisha kuwa inajenga mazingira mazuri ya kuimarisha usalama kwa
wageni wote wanaoingia hapa nchini.
Naye
Kamishna wa Polisi Zanzibar CP Mussa Ali Mussa, amesema kuwa kuanzishwa
kwa mafunzo hayo ya kikosikazi cha Utalii, kunatokana na mawazo ya Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Janerali Saidi Mwema, ya kuanzisha
kwa cha Polisi kinachoshughulikia masuala ya Utalii.
Kamishna
Mussa amesema kuwa Mafunzo hayo ambayo yana baraka zote za Rais wa
Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein, yamewajengea wahitimu hao uwezo wa
kiutendaji na moyo wa kuaminiana kati ya askari wa kikosi kimoja na
kingine pamoja na wale wa kamishneni ya Utalii.
Awali
Mkuu wa Chuo cha Taalum ya Polisi Zanzibar SSP Ramadhani Mungi, alisema
kuwa washiriki wa mafunzo hayo wamepatiwa mafunzo mbalimbali yakiwemo
ya ukamataji salama, Polisi Jamii pamoja na lunga mbalimbali za kigeni
kama vile Kiingereza, Kifaransa, Kitaliano na Kispanyola lugha ambazo
zitawawezesha kuwasiliana vema na wageni wanapokuwa na matatizo ama
kutaka kujua jambo kutoka kwao.
Amesema
wakufunzi wa Chuo cha Jeshi la Polisi Zanzibar pia wamepata msaada wa
kitaaluma kutoka kwa wakufunzi wenzao wa Chuo cha Maendeleo cha Utalii
kilichopo Maruhubi nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Kwa
upande wake, Mkufunzi Mkuu wa Chuo hicho ASP Ali Abdallah Kitole,
amesema kuwa majukumu makubwa ya askari hao ni kusaidia kuzuia uhalifu
dhidi ya watalii, kubainisha, kuzuia na kushughulikia uhalifu na jinsi
ya kutawala kiusalama eneo lenye watalii wengi.
Nao
baadhi ya wawekezaji na viongozi mbalimbali wa Kamisheni ya Utalii
Zanzibar wameelezea matumaini yao kwa Serikali ya Tanzania katika
kujiimarisha kwa ulinzi wa watalii hapa nchini.
MELI ZAFUTWA ZANZIBAR
Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi Zanziba
SERIKALI
ya Mapinduzi ya Zanzibar, imezifutia usajili meli tatu za abiria baada
ya kuonekana kuwa zinaweza kuhatarisha usalama wa abiria waacha kutoa
huduma za usafiri majini ili kuepuka ajali.
Meli
zilizofutwa ni Seagull, MV Kalama ambayo ni meli pacha na Mv Skagit
iliyozama baharini wiki iliyopita na MV Sepideh ambazo zote zilikuwa
zikifanya safari zake kati ya Zanzibar na Dar es Salaam na Zanzibar na
Pemba.
Uamuzi
wa kuzifutia usajili meli hiyo umetangazwa leo na Kaim Mkurugenzi wa
Mamlaka ya Usafiri Baharini Zanzibar (ZMA) Bw. Abdullah Hussein.
Kufuatia
uwamuzi huo, Serikali ya Mapinduzi ya Sanzibar, imetoa siku 30 kuanzia
leo kwa wamiliki wa Meli hizo wawe wameshaziondoa meli zao kwenye
maegesho ya meli Bandarini ili kutoa nafasi ya meli halila kuegeshwa
bandarini hapo.
Hatua
hiyo imekuja siku chache tu baada ya kuzama kwa meli ya Skagit na
kusababisha vifo vya zaidi ya abiria 100 na wengine 146 kunusurika baada
ya kuokolewa na wazamiaji wa vyombo vya ulinzi na usalama, mamlaka ya
Bandari na wapoigambizi wa makampunu binafsi.
Wakati
huo huo, hadi wakati natuma taarifa hizi, maiti zilizooolewa zimefiukia
123 baada ya kupatikana kwa maiti nyingine 17 na nyingine tano
kupatikana na kuzikwa kwenye fukwe za Pwani ya Bagamoyo mkoani Pwani.
No comments:
Post a Comment