Saturday, September 15, 2012

UKOSEFU WA AJIRA NI JANGA LINALOLIKABILI TAIFA-WASSIRA

SERIKALI imeunga mkono wazo la waziri mkuu mstaafu Edaward Lowassa kwa kukiri kuwa endapo hakutakuwa na mkakati thabiti wa kushughulikia tatizo la ajira kwa kundi la vijana kuna hatari kubwa ya kuleta machafuko katika siku za usoni.

Kauli hiyo ilitolewa na juzi wilayani Meatu na waziri wa nchi ofisi ya Rais Muhusiano na Uratibu Stephen Wassira wakati akizungumza na viongozi wa wilaya hiyo ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake mkoani Simiyu.

Kauli ya waziri Wassira imekuja kukiwa na kauli kadhaa ambazo zimekuwa zikitolewa na waziri mkuu mstaafu na mbunge wa Munduli Edaward Lowassa kuwa tatizo la ajira kwa vijana ni sawa na bomu.

Akizingumza na viongozi wa Meatu mbele ya wajumbe wa kamati ya ulinzi wakiongozwa na mwenyekiti wake Rossemary Kirigini,Wassira alisema kuwa tatizo la ajira kwa kundi la vijana ni kubwa sana na kwamba linatishia amani hivi sasa.

“Asilimia 60 ya watanzania ni vijana na hawana ajira hivi unategemea nini ndio maana wakiambiwa kuna maandamano wao hawaulizi maandamano hayo ni ya nini wanachouliza yananzia wapi na kwenpi tu”alisema na kuongeza.

“Hatuwezi kuwa taifa huku kundi kubwa la watu ambao ni vijana halina kazi hivyo kama viongozi lazima sasa tuchukue hatua mbalimbali kwa kutumia fursa tulizo nazo ili tuhakikishe tunapambana na changamoto hii”alisema Wassira.

Kwa sababu hiyo alitaka kupitia Tasaf awamu ya tatu pamoja na kulenga kuwezesha familia masikini kwaajili ya kuwangezea kipato ili kupambana na umasikini lakini pia halmashauri nchini kote zihakikishe zinahamasisha uundwaji wa vikundi vya vijana vya uzalishaji mali ambavyo vitawezeshwa ikiwa ni njia moja wapo ya kukabiliana na changamoto hiyo.

Alisema kama serikali imechukua hatua mbalimbali ambazo zitawezesha kukabiliana na tatizo hilo la ajira kwa vijana hasa kwa kutumia mkakati wa Kilimo Kwanza ambapo baada ya vijana kujinga katika vikundi watawezeshwa kupata zana za kisasa za kilimo ili kumudu kulima kisasa na kuzalisha kwa tija na kupata kipato kwaajili ya kupambana na umasikini.

Waziri Wassira,alisema kuwa katika kuwezesha makundi maalum katika jamii yasiyo na uwezo,tasaf awamu ya tatu itaanza kwa majaribio kwa wilaya za Bagamoyo,Kibaha na Chamwino kabla ya mpango huo kusambazwa nchini kote.

Kuhusu ukame ambao unaikabili wilaya hiyo,wasiri huyo alishauri viongozi kuanza kahamasisha kilimo cha Mtama ambao umekuwa ukivumia ukame badala ya kuendelea na kilomo cha za la mahindi.

Alisema kilimo cha zao la mtama kiende sambasamba kilimo cha zao la alizeti ambapo mbali na mtama kutumika kama chakula lakini zao la Alizeti linaweza kuwa zao mbadala la biashara badala ya kung’ang’ania kilimo cha zao moja la pamba ambalo limekuwa likiwaathiri wakulima bei inaposhuka katika soko la dunia.

Wakati huo huo waziri Wassira,alisema serikali ya chama cha mapinduzi CCM,kuwa iko tayari kutoa vibali vya ununuzi wa zao la pamba kwa mtu ama  kwa taasisi yoyoyote ambayo itaweza kununua zao hilo kwa bei ya juu ili kuondoa dhana kuwa serikali ndio inayohusika na kushuka kwa bei ya zao hilo katika msimu huu.

Akizungumza katika kijiji cha Nkololo wilayani Bariadi Wassira,wakati akihutubia wananchi wa kijiji hicho,alisema baada ya bei ya zao hilo kushuka katika soko la dunia,kuna baadhi ya watu wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa wamekuwa wakiwadanganya wananchi kuwa serikali ya ccm ndio inayohusika na kushuka kwa bei ya zao la pamba wakati wakitambua wazi serikali haina uwezo  huo.

Hata hivyo amerudia wito wake wa kusema njia pekee ya kuondokana  tatizo la kushuka kwa bei ya zao pamba kila wakati,ni  muda muafaka sasa wa kuweka wa makusudi kwa wamiliki wa viwanda vya kuchambua pamba kuanza kutengeneza nyuzi na nguo jambo  ambalo pia litamkomboa mkulima wa zao hilo.

No comments:

Post a Comment