Monday, May 19, 2014

Mbatia kutoa milioni 10 kwa professor atakayepata majibu yote sahihi ya mtihani wa darasa la 7

Changamoto ya mapungufu yaliyotajwa kwenye maandalizi ya vitabu na mitihani ya kumaliza darasa la saba imepelekea mheshimiwa James Mbatia kuwa-challenge maprofesa walioko bungeni kuufanya mtihani wa darasa la saba ambao kwa mujibu wake haufanyiki.
Akitoa mchango wake bungeni wakati wa mjadala kuhusu bajeti ya wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi ya mwaka 2014/2015, Mbatia amesema alichukua mtihani wa darasa la saba na kuupeleka kwa professor wa chuo kikuu cha Dar es Salaam na alimrudishia majibu kuwa mtihani ule haufanyiki.

“Njoo kwenye mtihani wa hisabati, na mimi napenda sana hisabati. Mheshimiwa spika, nilipeleka mtihani huu kwa professor wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, mtihani wa darasa la saba. Professor ameniandikia hapa ‘nimetumia muda wa  saa mbili na dakika tatu kufanya mtihani huu bila kuandika majibu kwenye karatasi na mtihani wenyewe haufanyiki.  Yaani ni madudu matupu yako kwenye mtihani huu. Nawachallenge wenzangu ambao ni maprofesa na wengine wanajua hisabati, wafanye mtihani huu waweze kupata 100/100 na mimi ntawapa shilingi milioni 10 ndani ya bunge hili.” Amesema James Mbatia.

Mbatia aliendelea kuweka msisitizo kuwa angeweza kuuweka mtihani huo kwenye meza bungeni hapo na professor yeyete ambaye ataweza kuufanya na kupata 100/100 angempa shilingi milioni 10.
Ameukosoa vikali mpango wa ‘matokeo makubwa sasa’ ambao amedai utekelezaji wake umegeuka kuwa madudu yanayotisha kwenye elimu ya Tanzania.

“Mheshimiwa naibu spika haya ni mambo ya kusikitisha, ni mambo ya kutisha. Na nchi yetu elimu ni dhaifu ya kupindukia. Elimu ni mapigo wa moyo ya taifa. Mapigo ya moyo yakienda kinyume na utaratibu wake maisha hupotea. Kwa hiyo uhai wa taifa la Tanzania hupotea kwa sababu tumeshindwa kuwekeza kwenye elimu. Wanafunzi wetu wanashindwa kufikiri yakinifu. Power of reasoning katika nchi yetu imekwenda chini sana kwa sababu elimu yetu ni dhaifu, ni dhaifu ya kutisha.” Ameongeza.

Amependekeza kuwa ili kupata tiba, bunge limuombe rais Jakaya Kikwete kuunda tume ya kudumu ya elimu nchini ambayo itakayokuwa inahakikisha ubora wa elimu na kudhibiti mambo yanayosababisha kutetereka kwa elimu nchini na amependekeza iitwe ‘Education quality assurance and control’.
.

No comments:

Post a Comment