Kikosi cha Taifa Starz
Dida shujaa wa Mchezo
......Bao la Stars limefungwa na John Bocco 'JB' dakika ya 16 kipindi cha
kwanza.......
|
Timu ya
Tanzania-Taifa Stars, ikicheza nyumbani kwenye uwanja wa Taifa Jijini Dar es
Salaam, May 18, 2014, imeifunga Zimbabwe bao 1-0 katika Mechi ya Kwanza ya
Raundi ya Pili ya Mtoano ya AFCON 2015 kuwania kucheza Fainali huko nchini
Morocco Mwaka 2015.
Katika Mechi
hiyo, bao pekee na la ushindi kwa Taifa Stars lilifungwa na Straika wa Azam FC,
John Bocco, katika Dakika ya 15 baada kuunganisha Krosi ya Thomas Ulimwengu
anaecheza TP Mazembe ya Congo DR.
Kocha wa Tanzania, Mholanzi Mart Nooij alisema baada ya mchezo huo kwamba
vijana wake wamecheza vizuri, lakini wangeweza kupata mabao zaidi kama
wangetumia vizuri nafasi walizotengeneza.
Kwa upande wake, kocha mzalendo wa Zimbabwe, Ian Gorowa alisema vijana
wake walicheza vizuri, lakini walikosa bahati ya kupata mabao licha ya kutengeneza
nafasi zaidi ya tatu nzuri.
Timu hizi
zitarudiana huko Harare Wikiendi ya kuanzia May 30,2014 na Mshindi atacheza na Mshindi kati ya
Mozambique na South Sudan kwenye Raundi inayofuata ambayo ndio itatoa Timu moja
kuingia KUNDI F kujumuika na Zambia, Niger na Cape Verde.
Katika mechi nyingine jana, mabao mawili ya Frank ‘Gabadinho’ Mhango
yaliipa Malawi ‘The Flames’ ushindi wa 2-0 dhidi ya Chad Uwanja wa Kamuzu mjini
Blantyre, nao Sao Tome Principe walifungwa 2-0 nyumbani na Benin, Namibia
iliilaza 1-0 Kongo na Mauritania iliibwaga 1-0 Equatorial Guinea.
AFCON
2015-MOROCCO: DROO YAFANYIKA.
DROO ya
Mashindano ya Mataifa ya Africa, rasmi kama Orange Africa Cup of Nations
Morocco 2015, ambayo Fainali zake zitachezwa huko Morocco kati ya Tarehe 17
Januari hadi 8 Februari 2015, imefanyika hii Leo huko Cairo, Egypt.
Nchi 51
zitashiriki Mashindano haya ambapo Mauritania na South Sudan zilishinda toka
Raundi ya Kwanza na kutinga Raundi ya Pili ya Mtoano ambayo Tanzania itacheza
na Zimbabwe.
Washindi 14
wa Raundi ya Pili ya Mtoano wataingia Raundi ya Tatu ya Mtoano ili kupata Timu
7 zitakazosonga kwenye Makundi ambayo hii Leo pia yamepangwa.
Ikiwa
Tanzania itaitoa Zimbabwe basi kwenye Raundi ya Tatu ya Mtoano itacheza na
Mshindi kati ya Mozambique na South Sudan na Tanzania ikipita hapo itaingia
KUNDI F ambako ziko Zambia, Cape Verde na Niger.
Yapo Makundi
7 ambapo Mshindi wa Kila Kundi na Mshindi wa Pili wa Kila Kundi pamoja na Timu
moja iliyofuzu Nafasi ya 3 Bora katika Makundi ndizo zitaingia Fainali kuungana
na Morocco na kufanya idadi ya Timu 16 kwenye Fainali.
RATIBA/MAKUNDI.
Nchi ambazo zimeingia Makundi moja kwa moja:-
Nigeria, Ghana, Ivory Coast, Zambia,
Burkina Faso, Mali, Tunisia, Algeria, Angola, Cape Verde, Togo, Egypt, South
Africa, Cameroon, DR Congo, Ethiopia, Gabon, Niger, Guinea, Senegal and Sudan.
RAUNDI YA PILI YA MTOANO.
Mechi Na 1: Liberia vs Lesotho
Mechi Na 2: Kenya vs Comoros
Mechi Na 3: Madagascar vs Uganda
Mechi Na 4: Mauritania vs Equatorial Guinea
Mechi Na 5: Namibia vs Congo
Mechi Na 6: Libya vs Rwanda
Mechi Na 7: Burundi vs Botswana
Mechi Na 8: Central African Republic vs Guinea Bissau
Mechi Na 9: Swaziland vs Sierra Leone
Mechi Na 10: Gambia vs Seychelles
Mechi Na 11: Sao Tome e Principe vs Benin
Mechi Na 12: Malawi vs Chad
Mechi Na 13: Tanzania vs Zimbabwe
Mechi Na 14: Mozambique vs South Sudan
**Mechi za Kwanza 16,17,18 Mei 2014
**Mechi za Marudiano 30,31 Mei au 1 Jun1 2014
RAUNDI YA TATU YA MTOANO.
**WASHINDI 14 wa Raundi ya Pili ya Mtoano watacheza Raundi hii
No comments:
Post a Comment