Saturday, November 30, 2013

Sfaxien yatwaa taji la CAF, Mbwana Samatta akiweka rekodi Afrika...

Mshambuliaji wa TP Mazembe, Mbwana Samatta
DR Congo, Lubumbashi
 
PAMOJA na kufungwa ugenini magoli 2 - 1 na TP Mazembe ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Club Sportif Sfaxien ya Tunisia imenyakua kombe la shirikisho barani Afrika kufuatia kushinda mechi ya mkondo wa awali kwa jumla ya magoli 2 - 0.
 
Mtanzania Mbwana Samatta aliyefunga bao la pili la Mazembe, ameweka rekodi baada ya kuwa Mtanzania wa kwanza kufunga bao katika mechi kubwa ya fainali kwenye michuano ya Afrika.
 
Mechi hiyo ya fainali mkondo wa pili imechezwa kwenye uwanja wa Lubumbashi Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
 
TP Mazembe wakijua wapo nyuma kwa magoli 2 - 0 waliofungwa katika mechi ya fainali mkondo wa kwanza walianza mchezo kwa kasi ambapo waliweza kusawazisha magoli yote mawili katika kipindi cha kwanza magoli yaliyofungwa na Chiebane Traore na Mbwana Samatta raia wa Tanzania.
 
Hata hivyo jitahata zao za kutaka kunyakua kombe hilo kwa mara ya kwanza zilizimwa katika ya 88 baada ya Fakhereddine Ben Youssef wa CS Sfaxien kupachika goli zuri kwa kichwa.
 
Hadi mwamuzi anapuliza fililmbi ya mwisho TP Mazembe ikawa imeifunga CS Sfaxien magoli 2 - 1
Kwa matokeo hayo na yale ya mkondo wa kwanza wa fainali hiyo CS Sfaxien ikawa imeiadhibu TP Mazembe kwa jumla ya magoli 3 - 2.
 
CS Sfaxieni wananyachukua kombe hilo kwa mara ya tatu baada ya kulinyakua mwaka 2007 na 2008 . TP Mazembe ilikuwa ikijaribu kunyakua kombe hilo kwa mara ya kwanza lakini ndoto hizo zimezimwa na Club Sportif Sfaxien.
 
TP Mazembe pamoja na kushindwa kunyakua kombe hilo la shirikisho barani Afrika, imeshanyakua kombe la Klabu Bingwa bara Afrika kwa mara kadhaa.
 
Mshindi wa kombe hilo Club Sportif Sfaxien ya Tunisia pamoja na kunyakua kombe hilo pia klabu hiyo imepewa kitita cha Dola za Kimerekani 660,000, ambazo ni zawadi kwa bingwa wa kombe hilo.
 
Vile vile CS Sfaxien itakutana na Klabu Bingwa barani Afrika Ahly ya Misri mwaka kesho katika kombe la maalum la "CAF Super Cup".

No comments:

Post a Comment