Saturday, November 30, 2013

Wajasiriamali nchini watakiwa kuwa na mikakati ya Pamoja kuuza bidhaa zao nje

  MUSOMA
 
Serikali imewataka Wajasiriamali wadogo kuwa na Mkakati wa Pamoja katika kuhakikisha bidhaa mbalimbali za Tanzania zilizoongezwa thamani zinauzwa nje ya nchi.
 
Kauli hiyo ilitolewa na  Waziri wa Kazi na Ajira Bi Gaudencia Kabaka katika ufunguzi wa Maonyesho ya Kanda ya Ziwa ya Viwanda vidogo vidogo Sido kwa Mwaka 2013  katika viwanja vya shule ya Msingi Mkendo manispaa ya Musoma mkoani Mara.
 
 Bi Gaudencia Kabaka- Waziri wa Kazi na Ajira
 
Alisema kitendo cha kupeleka Malighafi nje ya nchi husababisha kukosekana kwa ajira hapa nchini na hivyo kuwataka wafanyabiashra wadogo kuweka mkakati wa pamoja kuuza bidhaa nje ya Tanzania na si Malighafi.
 
" Tushirikiane kwa pamoja katika kuhakikisha bidhaa zetu zinauzwa nje ya nchi na si tupeleke Malighafi maana tunapeleka na ajira za watu" alisema Waziri Kabaka 
Waziri kabaka akikagua banda la Sido
 
Katika hatua nyingne Waziri Kabaka aliwaomba wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wa Halmashauri nchini kuwatambua WajasiriaMali katika Maeneo yao, kuwaongezea ubunifu na kuwatengea Maeneo ya kufanyia shughuli zao.

Awali akimkaribisha Waziri Kabaka,Kaimu Mkurugenzi wa Sido Bw Pius Wenga aalisema bidhaa za Tanzania zilizopo katika Maduka na Supermarket bado ni chache ikilinganishwa na nchi jirani.
 
Mapema katika ufunguzi huo Wazir kabaka alikagua mabanda mbalimbali katika Maonyesho hayo ya Kanda ya Ziwa ya Sido  ambayo yameelezwa ni  ya tatu kufanyika Mkoani Mara ambapo yalifanyika kwa Mara ya Kwanza mwaka 2004,2008  na 2013.
 
Waziri kabaka katika Picha tofauti

No comments:

Post a Comment