Belensi Alkaid-Mwanahabari Mara
George Marato-Mwanahabari Mara
Florence Focus -Mwanahabari Mara
Shomar Binda-Mwanahabari Mara
Mwenyekiti wa MRPC Emanuel Bwimbo kushoto na Kaimu katibu wa MRPC Raphael Okello Kulia
Waandishi wa habari nchini wameaswa kupendana ikiwa ni mikakati
ya kuendeleza taaluma hiyo pamoja na kuthamini Kazi ya Uandishi wa habari hapa
nchini.
Kauli hiyo imetolewa na
Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari Mkoani Mara (MRPC) Emanuel Bwimbo
katika Bwalo la Polisi mjini Musoma mkoani Mara Ikiwa ni Maadhimisho ya siku ya
Uhuru wa Vyombo vya habari duniani
ambayo hufanyika kila Mwaka Mei 3.
Alisema taaluma ya habari
ni taaluma nyeti hapa nchini ambayo inategemewa na Jamii kubwa hasa iliyopo
Vijijini lakini baadhi ya Waandishi wa habari wamekuwa hawaithamini taaluma
hiyo na hivyo kupelekea Jamii kuiona ni taaluma ya Kawaida wakati ina unyeti
wake.
“Mimi nashangaa sana maana
hii taaluma ni nyeti sana hapa nchini na inategemewa na asilimia kubwa hasa
Vijijini lakini sisi waandishi wa habari hatuitahamini taaluma hii kwanini?”
alisema Bwimbo
Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo amelaani tabia ya Mkuu wa
Mkoa wa Mara John Gabriel Tuppa kwa tabia yake ya kuchagua vyombo vya habari
wakati akijua kuwa kufanya hivyo kunaleta matabaka kwa Waandishi wa habari.
Biwimbo alisema kuwa tabia
ya Mkuu wa Mkoa kuchagua vyombo vya habari mbali na kuleta Matabaka lakini pia
husababisha Mahusiano kati ya Waandishi wa habari na Ofisi ya Mkoa kuwa Mabaya
na hivyo kulaani kitendo hicho.
“Tunamshangaa sana Mkuu wa
Mkoa maana siku hizi amekuwa na tabia ya kuchagua vyombo vya habari lakini hiyo
haitoshi ameanzisha tabia nyingine akialikwa sehemu anawaeleza wahusika hao
vyombo vya habari vya kuita katika hili hatukubaliani nalo kama Waandishi”
alisema Bwimbo.
Wakichangia katika
Kongamano hilo baadhi ya Waandishi wa habari kutoka Mkoani Mara wamesema tabia
aliyoianzisha katika kubagua Vyombo vya habari si nzuri na hivyo kusema hatua
hiyo haitaleta Mauhusiano mema katika Mkoa wa Mara.
Waliongeza kuwa haitakuwa
rahisi Mwandishi wa habari kuandika habari ambazo Mkuu wa Mkoa anazitaka huku
wakiongeza kuwa wao watasiamam Misingi ya habari.
“Haiwezekani Mkuu wa mkoa
atake waandishi wa habari wafanye kile ambacho anakitaka yeye kwani kufanyaa
hivyo ni kukiuka Misingi ya uandishi wa habari”
Katika Kongamano hilo
Waandishi wa habari wamependekeza kukutana na Mkuu wa Mkoa wa Mara kujadili
hilo na baada ya hapo Chama cha Waandishi wa habari Mkoani Mara watatoa tamko.
Kwa upande wake Kaimu
katibu Mkuu wa Chama hicho kutoka Wilaya ya Bunda Mkoani Mara Raphael Okello alisema suala la Maadili
linapaswa kuzingatiwa katika taaluma ya habari ikiwa ni njia ya kuipa heshima
taaluma hiyo.
Alisema kumekuwepo na
baadhi ya Waandishi ambao wamekuwa wakikiuka Misingi ya taaluma ya habari na
hivyo kuendelea kuipaka Matope taaluma hiyo,aidha kuhusu baadhi ya wanahabari
wanaotumia nafasi hiyo kutisha jamii Kaimu katibu mkuu huyo alisema kuwa hiyo
ni tabia mbaya ambayo haipaswi kufumbiwa Macho.
“Baadhi ya Waandishi
wamekuwa wakiipaka Matope taaluma hii kwa kukiuka Maadili hivyo basi ni vyema
kila Mwandishi wa habari akafuata misingi ya taaluma hii ya habari” alisema
Okello
No comments:
Post a Comment