Friday, May 3, 2013

KATIBU MKUU WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI AFUNGUA KONGAMANO LA WAANDISHI WA HABARI ARUSHA

images

……………………………………………………..
Katibu Mkuu wa jumuiya ya Afrika ya mashariki  Dr. Richard Sezibera  amefungua rasmi kongamano la waandishi wa Habari Tanzania pamoja nchi wanachama wa jumuiya ya afrika ya mashariki katika kuadhimisha ya uhuru wa vyombo vya Habari Diniani uliobeba kauli isemayo USALAMA NA MAZINGIRA BORA YA KUFANYIA KAZI KWA WAANDISHI WA HABARI NA WAHARIRI AFRIKA YA MASHARIKI.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kaongamano hilo la waandishi wa habari liliofanyika jijini hapa katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Naura Spring  amesema kuwa kongamano hili la vyombo vya Habari pamoja na wamiliki lina umuhimu kwa sababu litaifanya jamii pamoja na serikali kujua nini umuhimu wa uhuru wa vyombo vya habari katika maendeleo ya nchi na jamii yote.

Amesema kuwa uhuru wa  vyombo vya habari kwa kiasi kikubwa unajikita katika uhuru wa kutoa maoni na pamoja na uhuru wa  kutoa habari  hivyo katika kuelewa hilo vyombo vya habari vinatakiwa viwe vinafanya kazi zake pasipo kuegemea upande wowote ili kusije kuchochea kuvunja amani ya nchi kama ilivyotokea miaka ya nyuma kwa nchi ya Rwanda na Burundi.

Aidha amesema kuwa kuna changamoto kubwa sana zinazovikumba vyombo vya habari hususani vyombo vya kijamii  ambapo wanakuwa na mazingira magumu ya kutafuta habari na kufanya wakati mwingine waandishi kuwa katika mazingira hatarishi  kwa maisha yao pamoja na hali mbaya ya kiuchumi inayopelekea kutoweza kufanya kazi kuendana na mabadiliko ya sayansi na Technolojia ikiwepo kujiingiza katika mawasiliano ya mkongo wa kimtaifa.

Kongamano la mwaka huu limeratibiwa na  MISSA TANZANIA kwa kushirikiana na  EAJA, Mfuko wa vyombo vya Habari Tanzania ( TMF), Muungano wa klabu za wandishi wa habari (TPC), Umoja wa Mataifa Tawi la Tanzania, Baraza la Habari Tanzania (MCA), Wamiliki wa Vyombo vya habari Nchini (MOAT) pamoja na kituo cha habari kwa wananchi TCIB.

No comments:

Post a Comment