Thursday, May 2, 2013

Njama ya mapinduzi yatibuliwa Chad

Watu kadhaa akiwemo mbunge wa upinzani wamekamatwa katika mji mkuu wa Chad 

Ndjamena, katika kile ambacho serikali inasema ilikuwa njama ya kuvuruga hali nchini humo.

Taarifa kutoka kwa vyombo vya serikali zinasema kuwa kundi moja dogo la watu limekuwa likipanga njama hiyo kwa miezi minne.

Viongozi wa njama hiyo ya mapinduzi wanachunguzwa na viongozi wa mashtaka.

Chad ina historia ndefu ya mapinduzi na uasi. Rais wa sasa Idriss Deby mwenyewe alichukua mamlaka kwa njia ya mapinduzi mwaka 1990.

Serikali ilisema kuwa kundi moja la watu wenye nia mbaya walijaribu kufanya mapinduzi dhidi ya taasisi za nchi.

Ilisema kuwa maafisa wa usalama wa serikali walikabiliana nao bila kutaja idadi yao.

Polisi pamoja na duru za upinzani zilisema kuwa mbunge huyo Saleh Makki alikuwa miongoni mwa waliokamatwa.

Pamoja na waliokamatwa ni wanajeshi kadhaa,Tangu nchi hiyo kujipatia uhuru kutoka kwa Ufaransa, mwaka 1960, Chad imekumbwa na misukosuko hasa kati ya eneo la Kaskazini ambalo lina waarabu wengi na Kusini ambako kuna wakristo wengi.

Mapema mwaka huu Chad iliwapeleka wanajeshi 2,000 kujaribu, kuwatimua wapiganaji walioteka sehemu kubwa ya Mali.

No comments:

Post a Comment