Thursday, April 18, 2013

CHAMA CHA MAPINDUZI HAKIPOTAYARI KUWA NA KIONGOZI ASIYEFANYA KAZI-SANYA

 Mwenyekiti wa CCM Mkoani Mara Bw.Christopher Mwita Sanya katika mkutano na Wanahabari
 Emanuel Bwimbo kulia akiwa na Anna Mroso katika mkutano na Mwenyekiti wa CCM
 Katibu wa CCM Vijana  Mkoani Mara akiwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara
                                      CHRISTOPHER MWITA SANYA
    Shomar Binda akiwa katika pozi



MUSOMA  
  
Chama cha Mapinduzi mkoani Mara kimesema hakipo tayari kuwa na kiongozi ambaye  hatimizi wajibu wake kwa Wananchi  na hivyo kupelekea Wananchi kulalamika juu ya Serikali iliyopo Madarakani.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM mkoani Mara Bw. Christopher Mwita Sanya wakati akiongea na Waandishi wa habari mkoani hapa.

Amesema wabunge na Madiwani wa Chama hicho waliochaguliwa katika uchaguzi Mkuu mwaka 2010,Sanya amesema kuwa viongozi hao wanapaswa kutimiza kile walichokiahidi wakati wa Kampeni.
 
Kuhusu suala la Makundi ndani ya Chama hicho Mwenyekiti huyo amesema kwasasa suala hilo halina nafasi huku akieleza sababu ya kufanya vibaya Kwa baadhi ya Maeneo katika uchaguzi Mkuu uliopita.

Katika hatua nyingine Bw Sanya amewataka Vijana kutochagua kazi na kuamini Kilimo kama njia sahihi kufanikiwa katika Maisha.






No comments:

Post a Comment