Kanali Fabian Massawe. |
Kanali
mstaafu MASSAWE ametoa kauli hiyo mkoani Kagera alipokutana na wakurugenzi na
waandishi wa vyombo mbalimbali pamoja na wadau wa habari mkoani humo.
Maadhimisho
ya Siku ya Mashujaa hufanyika kila tarehe 25 mwezi Julai.
Kitaifa
mwaka huu yatafanyika Julai 25, mkoani
KAGERA, katika kambi ya Jeshi la Wananchi-JWTZ-KABOYA, wilayani MULEBA.
Mgeni rasmi
katika maadhimisho hayo atakuwa rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk JAKAYA KIKWETE.
Mkuu wa mkoa
wa KAGERA, Kanali mstaafu FABIAN MASSAWE, ameshauri vyombo vya habari na Wana
habari kuhamasisha jamii mkoani humo kujiandaa kikamilifu kwa ajili ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa.
|
Picha juu na
nichi ni baadhi ya waandishi habari wa vyombo mbalimbali wakifuatilia katika
mkutano huo uliowashirikisha wadau wa habari pia.
|
Kanali
MASSAWE amesema vyombo vya habari na
Wanahabari ni kiungo muhimu katika
kuhamasisha jamii iweze kushiriki kikamilifu katika maadhimisho hayo.
Ameshauri
Wazee walioshiriki matukio wakati ule
kujitokeza na kusimulia ili liwe
fundisho kwa jamii ya sasa itambue
uzalemdo wa kuipigania nchi yao.
Aidha
amewataka Wakazi wa mkoa wa KAGERA kutumia fursa hiyo kuwekeza zaidi na kupata
ajira.
No comments:
Post a Comment