Tuesday, April 30, 2013

MWANTUMU AWA SKAUTI MKUU – UTEUZI WA RAIS

images
RAIS wa Jamhuri ya Muungan wa Tanzania Dk. Jakaya Mrsho Kikwete amemteua Mh. Mwantumu Mahiza kuwa Skauti Mkuu nchini.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, uteuzi huo wa Mahiza umeanza Aprili 19 mwaka huu.

Balozi Sefue amesema Mh. Mwantumu Mahiza atatumikia nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka minne hadi Aprili 19 mwaka 2017.

Mh. Mwantumu Mahiza anakuwa Skauti Mkuu kuchukua nafasi ya Kanali Mstaafu Idd Kipingu aliyemaliza muda wake kutumikia nafasi hiyo.

Mh. Mahiza mbali na kushika wadhifa huo, pia anatumikia nafasi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani.

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE KUFUNGUA MKUTANO WA KILIMO.

images
Na Hassan Silayo na Lorietha Laurence
…………………………………………………….
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete anatarajia kufungu
a mkutano wa Kilimo wa Umoja wa Nchi za Kusini mwa Africa, utakaofanyika tarehe 13 hadi 14 Mei mwaka huu .

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mkutano wa Vyama vya Kilimo vya Kusini mwa Afrika (SACAU), Ishmael Sunga wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu mkutano huo utakao fanyika katika hoteli ya White sands iliyopo jijini Dare s salaam.

Alisema kuwa kipaumbele katika kipindi hiki ni kupambana na changamoto ya kilimo,na usalama wa chakula ili kufanya sekta ya kilimo kukua , kustawi na kufanya kilimo kuwa biashara badala ya kufikiri katika kuondoa umaskini.

“Lengo litakuwa ni kubadilisha mtazamo wa watu kuwa, kilimo ni kwa ajili ya kumfanya mkulima ajikimu mahitaji ya kawaida na kuondoa umaskini, bali ni kumfanya mkulima kupata faida na kutajirika kupitia kilimo katika ngazi zote za kilimo”, alisema Sangu.

Aliongeza kuwa mkutano huo una malengo ya kuwasaidia na kuwaongezea nguvu wakulima pamoja na kutoa taarifa za kilimo kwa wadau wa sekta hiyo kwa niaba ya wakulima wote wanachama wa umoja huo ili kuleta tija katika sekta hiyo muhimu ya kilimo.

Naye Mkurugenzi wa Baraza la Kilimo Tanzania Janet Bitegeko alisema baada ya mkutano huo washiriki watapata fursa ya kutembelea wakulima wa mpunga katika kijiji cha Bagamoyo ili kujionea changamoto na nini wakulima hao wanafanya na kutoa ushauri ili kuweza kuboresha zaidi zao hilo.

Janet aliongeza kuwa umoja huo utatoa taarifa za utekelezaji za mwaka pamoja na kufanya ukaguzi wa hesabu za mwaka za umoja huo.

Mkutano huo utahudhuriwa na washiriki kutoka nchi 14 wakiwemo wakurugenzi na wenyeviti kutoka nchi za kusini mwa afrika, wawakilishi zaidi ya 10 wa muungano wa wakulima pamoja na taasisi za kifedha.

Kauli mbiu ya mkutano huo ni kusaidia kilimo cha biashara na maendeleo ya biashara yanayolenga mkakati maendeleo ya kilimo katika nchi za kusini mwa afrika, ambapo waziri wa kilimo wa Nigeria atatoa kauli.

Wanajeshi kutoka nchini Nigeria waitembelea wizara ya Habari

picha no.2Katibu Mkuu wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Sethi Kamuhanda  (kulia) akiangalia picha ya nembo ya chuo cha Ukamanda na Unadhimu cha nchini Nigeria aliyopewa na Mkurugenzi wa kikosi cha Maji kutoka nchini Nigeria Meja Generali  Ati John (kushoto) alipomtembelea ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam. Jumla ya wanajeshi 22 kutoka chuo hicho wako nchini kwa  ziara ya mafunzo ya siku tano.PICHA NA ANNA NKINDA WA MAELEZO picha no.3Mkurugenzi wa kikosi cha Maji kutoka nchini Nigeria Meja Generali  Ati John (kushoto) akimwelezea Katibu Mkuu kutoka wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Sethi Kamuhanda  kuhusu picha ya kinyago kinachoonyesha mtawala wa makabila mbalimbali ya nchi hiyo alipomtembelea ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam. Jumla ya wanajeshi 22 kutoka chuo cha Ukamanda na Unadhimu cha nchini Nigeria wako nchini kwa  ziara ya mafunzo ya siku tano. picha no.4Katibu Mkuu wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Sethi Kamuhanda  (kulia) akimkabidhi picha ya wamasai Mkurugenzi wa kikosi cha Maji kutoka nchini Nigeria Meja Generali  Ati John (kushoto) wakati wanajeshi 22 kutoka chuo cha Ukamanda na Unadhimu walipomtembelea  ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam. picha no.5Katibu Mkuu wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Sethi Kamuhanda  (kulia) akimkabidhi picha ya kinyago cha ujamaa Mkurugenzi wa kikosi cha Maji kutoka nchini Nigeria Meja Generali  Ati John (kushoto) wakati wanajeshi 22 kutoka chuo cha Ukamanda na Unadhimu walipomtembelea  ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam. Wanajeshi hao kutoka nchini Nigeria wako ziara ya mafunzo ya siku tano nchini. picha no.6 Kanali Anderson Msuya (kushoto) kutoka Jeshi la Wananchi la wa Tanzania (JWTZ)  akiongea jambo na Mkurugenzi wa kikosi cha Maji kutoka nchini Nigeria Meja Generali  Ati John wakati wanajeshi 22 kutoka chuo cha Ukamanda na Unadhimu walipoitembelea wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Mchezo leo jijini Dar es Salaam. picha no.7Baadhi ya  wanajeshi 22 kutoka chuo cha Ukamanda na Unadhimu cha nchini Nigeria wakimsikiliza Katibu Mkuu kutoka wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Sethi Kamuhanda (hayupo pichani) wakati walipomtembea ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam. picha no.8jpgMkurugenzi wa Bodi ya Filamu na Michezo ya kuigiza Joyce Fisoo akielezea kuhusu kazi za bodi hiyo kwa wanajeshi 22 kutoka chuo cha Ukamanda na Unadhimu cha nchini Nigeria walipoitembelea wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Joyce Hagu ambaye ni Kaimu Mkurugenzi msaidizi Idara ya utamaduni. picha no.9Wanajeshi 22 kutoka chuo cha Ukamanda na Unadhimu cha nchini Nigeria wakiwa katika picha ya pamoja  na wafanyakazi wa wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakati walipoitembelea wizara hiyo leo jijini Dar es Salaam. Wanajeshi hao  kutoka chuo cha Ukamanda na Unadhimu wako nchini kwa  ziara ya mafunzo ya siku tano.

JAJI MKUU WA TANZANIA AMTEMBLEA SPIKA WA BUNGE OFISINI KWAKE DODOMA LEO

1Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akimkaribisha Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman alipofika kumtembelea Ofisini kwake Dodoma leo na kufanya nae mazungumzo.(PICHA ZOTE NA OWEN MWANDUMBYA WA BUNGE)
2 Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akifafanua jambo mbele ya Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman alipofika kumtembelea Ofisini kwake Dodoma
4 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman pamoja na ujumbe wake wakimsikiliza Spika wa Bunge Ofisi Kwake leo. Jaji Mkuu na Ujumbe wake walimtembelea Mhe. Spika na kufanya nae Mazungumzo Ofisini kwake Mjini Dodoma5Mbunge wa Maswa (CHADEMA) Mhe. John Shibuda akimsindikiza Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman kuelekea Ofisi ya Spika alipofika viwanja vya Bunge leo. Jaji Mkuu na Ujumbe wake walimtembelea Mhe. Spika na kufanya nae Mazungumzo Ofisini kwake Mjini Dodoma

KAMUHANDA -ELIMU YA UZALENDO IMECHANGIA NCHI KUWA NA AMANI NA UTULIVU           picha no.1Katibu Mkuu wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Sethi Kamuhanda  (kulia) akisoma jarida la Eagle alilopewa Zawadi na Mkurugenzi wa kikosi cha Maji kutoka nchini Nigeria Meja Generali  Ati John (kushoto) alipomtembelea ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam. Jumla ya wanajeshi 22 kutoka chuo cha Ukamanda na Unadhimu cha nchini Nigeria wako nchini kwa  ziara ya mafunzo ya siku tano.

…………………………………………………………….
 NA MAGRETH    KINABO
                                                                     
ELIMU ya uzalendo imesaidia  kuwafanya  vijana  wa Kitanzania kuipenda nchi yao , hali iliyochangia nchi yetu kuwa na amani na utulivu.
Kauli hiyo ilitolewa leo na  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana ,Utamaduni na  Michezo,Seth Kamuhanda wakati akizungumza na ujumbe wa  watu 22,baadhi yao ni viongozi wa utawala na 13 ni wanafunzi wa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu wa mafunzo ya   kijeshi  kutoka  Nigeria.
Ujumbe huo umetembelea wizara hiyo kwa ajili ya kujifunza masuala mbalimbali ya  Utamaduni wa Kitanzania, umeongozwa na kiongozi wa msafara, Meja   Generali, Ati  John,ambaye ni Mkurugenzi wa Jeshi la Wanamaji.
“Mojawapo ya program tunazowafundisha  vijana ili kuondoa  migogoro  katika nchi  yetu ni elimu ya uzalendo ,yaani tunawafundisha jinsi ya kuipenda nchi yao.  Elimu hii imesaidia  kupunguza migogoro,alisema.” Katibu Mkuu huyo alipokuwa akijibu swali la mmoja ya wanafunzi  hao   lililouliza kuwa  kuna program  zipi zinazochangia kupunguza migogoro  hususan kwa vijana.
Katibu Mkuu huyo aliongeza kuwa kuna mkakati wa kuwawezesha vijana kiuchumi ili waweze kubuni miradi mbalimbali kwa kuwa na mfuko wa vijana.
Alisema katika mpango huo vijana wanakuwa katika vikundi na kufanya shughuli  mbalimbali  kuwawezesha kiuchumi.
Aidha Katibu Mkuu huyo akizungumza kuhusu masuala ya kiutamaduni ,alisema wizara  yake ndi yenye jukumu lakuendeleza Utamaduni wa Mtanzania, hivyo katikawizara hiyo yenye sekta nne, ambazo ni Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
 Kamuhanda  alisema sektaya utamuduni ndio inayofanyakazi ya kudumisha Utamaduni huo.
 Aliongeza kuwa lugha ya Kiswahili ndio imekuwa lugha kuu ya mawasiliano nchini  na ndiyo iliyoleta umoja ,amani na mshikamano.
 Wakizungumzia kuhusu ziara hiyo kiongozi huyo na mmoja wa wanafunzi,  Ikema Francis walisema wameshukuru kwa taarifa walizopata kuhusu wa masuala hayo ya kiutamaduni na kuhafamu kuwa lugha ya Kiswahili ndiyo imeleta umoja.

No comments:

Post a Comment