Musoma
WATU watatu
wamefariki dunia katika matukio matatu tofauti yakiwemo ya kuawa,kujinyonga na
kuchomwa kisu mkoani Mara.
Katika tukio
la kwanza lilotokea juzi watu wenye hasira katika kijiji cha Nyabirekera
wilayani Serengeti,wamemuawa mkazi mmoja wa kijiji hicho kwa kipiga mawe kisha
kuuchoma moto mwili wake baada ya kumtuhumu kujihusha kwa imani za kishirikina.
Kamanda wa
polisi mkoani Mara,kamishna Msaidizi Mwandamizi Absalom Mwakyoma,alimtaja
marehemu kuwa ni Nyabuke Maheri,ambaye anakisiwa kuwa na umri wa miaka 68.
Hata hivyo
kamanda Mwakyoma,alisema ingawa bado chanzo cha tukio hilo kinachunguzwa lakini
ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi badala
yake wanapowakamata wahalifu kwa makosa yoyote wawafikishe katika vyombo dola
ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.
Katika tukio
lingine ambalo limetokea wilayani Tarime,kamanda wa polisi wa mkoa wa kipolisi
wa Tarime na Rorya Justus Kamugisha,alisema mtu mmoja Genkuri Chacha(34)
aliuawa baada ya kuchomwa kisu na mdogo wake Nyengwe Chacha(25).
No comments:
Post a Comment