MWANAMKE AUAWA KISHA KUCHOMWA MOTO
AKITUHUMIWA KUHUSIKA NA KIFO CHA JILANI YAKE
.
“Baada ya kufa jilani yake maiti
ikapelekwa kwa
mtuhumiwa,wakachoma nyumba kisha wakampiga
na kumteketeza kwa moto”
-Serengeti.
Februari 4,2013.
MWANAMKE
mmoja mkazi wa kitongoji cha Stooni kijiji cha Nyiberekera kata ya Issenye
wilayani Serengeti ameuawa kisha mwili na nyumba yake kuteketezwa kwa moto na
wananchi kwa tuhuma za kujihusisha na ushirikina.
Tukio
hilo limetokea februari 2 ,majira ya saa 9:00
arasili nyumbani kwake mwaka huu
baada ya kufariki mkazi mmoja kijijini hapo na maiti kutelekezwa kwa mama huyo
wakimtuhumu kuhusika na kifo hicho limethibitishwa na uongozi wa kata na polisi
wilayani hapa.
Kwa
mjibu wa habari zilizolifikia Mwananchi na kuthibitishwa na diwani wa kata hiyo
Ally Nyarobi zinadai aliyeuawa na mwili wake kuteketezwa kwa moto na kundi la
wananchi ni Nyabuke Mese (50).
Diwani
alisema kuwa kabla ya wananchi kufanya unyama huo kulitokea kifo cha mkazi
mmoja kwenye kitongoji hicho Kikene Kasinge(40)ambacho mama huyo alihusishwa na
maiti kupelekwa nyumbani kwake .
“Mama
huyo alihusishwa na kifo cha Kasinge kwa kile kinachodaiwa kuwa alimroga na
maiti ikapelekwa kwake wakati hayupo…wakaweka maiti hapo kisha wakachoma moto
nyumba yake …alipoona hali hiyo akajitokeza na katika mahojiano akajibu kuwa
pamoja na kuchoma nyumba atajenga na hawamfanyi kitu … wakampiga kisha
wakamchoma moto na kuteketea ”alisema diwani.
Mashuhuda wanena.
Baadhi
ya mashuhuda walioongea na Mwananchi kwa kutokutajwa majina yao gazetini walisema mapema wiki hii mama huyo alimkuta
Kasinge nyumbani kwa Greta Chibagi akinywa pombe ya kienyeji aliyonunua kwa
tsh,300 na kumlazimisha wakae naye na ampe pombe.
“Kasinge
alikataa kwa madai kuwa mama huyo ametengwa na jamii kutokana na vitendo vyake
vya ushirikina ,watu hawaendi kwake…alimjibu kuwa kama wamenitenga ndani ya
siku tatu wewe utakuja kwangu na wengine watafuata”alisema shuhuda .
Alibainisha
kuwa kauli hiyo ilimfanya Kasinge atoke eneo hilo,hata hivyo mama huyo
alimfuata njiani na kumtaka aende naye kwake nay eye akakataa,lakini akazidi
kumwambia kwa njia yoyote lazima atakwenda na kumpa siku 3 tena.
“Januari
30 akaugua ghafla homa kali akapelekwa zzahanati kupimwa akaonekana hana ugonjwa
huku hali ikizidi kuwambaya…ajabu akawa bubu …januari 31 akapelekwa kwa mganga
wa kienyeji kijijini hapo ambaye ni mgeni akawaambia hana uwezo wa kutibu
ugonjwa huo..februari 2,majira ya saa 6:00 mchana akakata roho”alisema shuhuda.
Matukio mengine aliyowahi kuhusishwa
nayo.
Vyanzo
hivyo vilisema kuwa mama huyo amewahi kukiri mbele ya mkutano wa kitongoji
hicho ulioitishwa chini ya Mwenyekiti wake Makuru Siboti kuwa ameishaua watu
wanane wa familia moja.
Na
kuwa alifikishwa polisi Issenye kisha Mugumu lakini alichiwa kutokana na
udhaifu wa sheria ya Uchawi ya mwaka 1928 ambayo hata watendaji wa serikali
hawaijui na namna ya kushughulikia masuala yanayohusishwa na vitendo vya
kishirikina.
Mbali
na hilo pia aliwahi kubanwa kwa tukio la kumtishia Greta Sarota mkazi wa
kijijini hapo kuwa mwanae aliyekuwa kidato cha pili Nagusi Sekondari kuwa ana
akili atamkomesha.
“Haikuchukua
muda mtoto huyo akapotea katika mazingira ya kutatanisha na alipobanwa huyo
mama mtoto akarudi lakini akiwa hataki shule mpaka sasa”mwananchi iliambiwa.
Alihusika mgogoro wa kugombea Fisi wa
uchawi.
“Mwishoni
mwa mwaka jana na Mwanzoni mwa mwaka huu huyo mama alihusika katika mgogoro wa
kugombea fisi uliomhusisha Mirengali Kitoshi na kijana mmoja wa kijaluo”alisema
mkazi wa kitongoji hicho jina limehifadhiwa.
Katika
mgogoro huo Mirengali alimfikisha ofisi ya serikali ya kijiji kijana huyo
akidai ni jambazi na ndipo akatoboa siri kuwa ugomvi wao unahusu fisi wa uchawi
aliyepewa kwenda naye kijijini kwao Rorya na kufika huko akaokoka na fisi akawa
amekufa kufuatia chumba alimokuwa amemweka walipuliza dawa ya ukoka.
Kijana
huyo ambaye alikuwa kijijini hapo kwa shughuli za kibarua cha kuchunga mifugo
alimtaja mama aliyechomwa moto kuwa ndio walikuwa washirika,ambao walimtaka
amtoe mama yake kafara baada ya kupoteza fisi wao wa kazi,hata hivyo alifukuzwa
kijijini hapo.
Maiti iliyotelekezwa yachukuliwa na
polisi.
Polisi
wilayani hapa walilazimika kuchukua maiti ya Kasinge ambayo ilitelekezwa
nyumbani kwa mama huyo aliyechomwa na imehifadhiwa chumba cha Maiti hospitali
teule ya Nyerere ddh .
Hospitali wathibitisha kupokea maiti ya
Kasinge
Mganga
mkuu wa hospitali teule ya Nyerere ddh Dk,Kelvin Mwasha amekiri kupokea mwili
wa Kasinge ambao ulipelekwa na polisi,ingawa hawajaambiwa nini kinatakiwa kwa
kuwa hata polisi hadi tunakwenda mitamboni walikuwa hawajafika hospitali
kueleza kinachotakiwa kufanyika.
Ndugu na familia walazimika kuzika mama
aliyechomwa.
Katika
hali inayoonyesha wananchi kuchukizwa na matendo ya mama huyo hata kwenye
mazishi yake hawakuhudhuria bali ndugu
na wanae ndio waliohusika.
Hakuna
mtu anayeshikiliwa kuhisiana na tukio hilo na polisi wanadai wanaendelea na
uchunguzi huku ndugu wa marehemu Kasinge wakisubiriwa ili kuchukua mwili wa
ndugu yao walioutelekeza nyumbani kwa Nyaboke ambaye aliuawa.
No comments:
Post a Comment