Monday, February 4, 2013

SERIKALI YASEMA HAITAWAVUMILIA WANASIASA WANAOCHOCHEA VURUGU






  Mkuu wa mkoa wa Mara Bw John Tuppa
MUSOMA

Serikali mkoani Mara imewataka  wanasiasa waache kutumia Jukwaa  la siasa kuchochea chuki,vurugu huku wakihamasisha wananchi kuvunja sheria za nchi.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Mara  John Gabriel Tupa,wakati wa kukabidhi piki piki 12 kwa wilaya nne za mkoa wa Mara ambazo zimetolewa na Serikali kwaajili ya kusadia suala la ulinzi katika mradi wa ukaguzi wa tarafa.

 Mkuu huyo wa Mkoa ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Mara amesema viongozi  wa vyama vya siasa  wakiwemo na viongozi wa madhebu ya dini watumie nafasi  zao kuhubiri upendo na amani miongoni mwa jamii pamoja na kuheshimu sheria za nchi.


Mbali na kauli hiyo Mkuu huyo wa mkoa amesema Mkakati wa Jeshi la Polisi ni kuzuia Uhalifu na Kujenga mahusiano na Jamii na kuongeza kuwa Pikipiki hizo zisitumike katika matendo yasiyofaa.

Kwa upande wake  kamanda wa polisi mkoa wa Mara kamishna msaidizi wandamizi Absalom Mwakyoma,amesema piki piki hizo ni sehemu piki piki 164 za ukaguzi wa tarafa kwa kuzuia uhalifu mradi ambao uliziinduliwa na mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Said Mwema January 11 mwaka huu lengo likiwa ni kupambana na wahalifu na uhalifu hapa nchini.

Wilaya zilizoweza kupata pikipiki hizo ni wilaya za Serengeti,Bunda,Musoma mjini na wilaya ya Butiama

No comments:

Post a Comment