Hapa watu wanachakarika kiwandani ndani kazi hakuna kulala
Tukiwa kiwandani na mwenyeji wetu B Joseph Mathayo tukauza sura kidogo mm na Shom B
Hapa nikitazama moja ya Mashine ambayo ni mpya kiwandani hapo
Mkurugenzi wa Kiwanda huyo Bw Joseph Mathayo akizidi kutupatia maelezo
Safi kazi inaendelea
Hapa tukiangalia Pamba ambayo tayari imeishwa tengenezwa yaani ni safi
Tunazidi kupata ufafanuzi zaidi kutoka kwa ndugu Joseph Mathayo
Umakini unatakiwa wakati wa Maelezo
Hapa ni sehemu ya kusaga Mbegu zilizochambuliwa
Jamaa wakaamua kuweka Pozi
Si mbaya kuweka Pozi
Haya ni Mafuta ambayo yanazaliwa kiwandani hapo
Mashudu kwa ajili ya chakula cha Ngo'ombe
Tulikuta baadhi ya Pamba safi ikiwa tayari na hili ni moja ya gari ambalo lilikuwa tayari kupakia kuelekea Jijini DSM
Bw Joseph Mathayo (Rambo) ambaye ni mkurugenzi wa kiwanda hicho
Augustine Mgendi
BUTIAMA
Kiwanda cha Pamba cha Mgango Ginnery kilichopo katika eneo la Mgango wilaya ya Butiama
Mkoani Mara kimeendelea kujenga Mahusiano Mazuri na Wakulima kutoka mikoa ya
Mara,Mwanza na Simiyu kuwaendeleza katika zao la Pamba.
Akiongea na
Waandishi wa habari waliotembelea kiwandani hapo,Mkurugenzi wa kiwanda hicho
Joseph Mathayo alisema kuwa kiwanda
hicho kimeanza uzalishaji mwezi Julai mwaka huu ambapo msimu rasmi ulianza
mwezi Juni.
Alisema
Mpaka sasa Mapokeo ni Mazuri kwa wananchi mbalimbali kutoka Mikoa ya
Mara,Mwanza na Simiyu kitu kinachowapa nguvu ya kuendelea na uzalishaji wa
Pamba,chakula cha Mifugo na Mafuta ya kupikia.
“Kwasasa ndiyo tunaanza Msimu wetu kwa mara ya
kwanza maana tunachojivunia mpaka muda huu ni kuwa mapokeo ni mazuri ya wakazi
wa mikao ya Simiyu,Mara na Mwanza.”alisema Mkurugenzi huyo.
Mkurugenzi
huyo alisema kuwa kulikuwa na tabu kubwa wakati wa kuanza msimu kwani Wakulima
wengi hawakuwa na mtaji hivyo upatikanaji wa Pamba ukawa shida.
Bw Joseph
Mathayo ambaye alijivunia ubora wa Mafuta ya kupikia yanayozaliwa na Kiwanda
hicho ya nayofahamika kwa jina la Mafuta ya Radha alisema kuwa Mafuta hayo ni
meupe ikilinganishwa na Mafuta mengine yaliyopo Sokoni.
“Mafuta yetu ni Meupe sana na hii inatokana na
ubora ambao tunautumia katika kuyatengeneza hivyo ni wananchi kuyajaribu kasha watupe
majibu” alisema Bw Joseph Mathayo maarufu kwa jina la Rambo.
Alisema
mpaka sasa kiwanda kimeajiri wafanyakazi 55 ambapo uwezo ni kuajiri wafanyakazi
70 huku vibarua wakiwa 120,Bw Mathayo aliongeza kuwa mpaka sasa zipo awamu tatu
za kazi na kueleza jinsi wanavyogawa mbegu kwa wakulima na kasha kuwapa madawa.
Akiongelea
changamoto zilizopo alisema ni pamoja na Miundombinu iliyopo kwasasa huku
changamoto nyingine ilikuwa ni upatikanaji wa vibali wakati kwa kuanza.
Pamoja na
changamoto hizo Mkurugenzi huyo alisema kuwa wananchi wa Mikoa ya Kanda ya ziwa
wanaombwa kushirikiana na Kampuni hiyo ili kuendelea kuzalisha lakini kubwa
zaidi ni kuendelea kutoa ajira kwa Watanzania.
“Nadhani kikubwa ni kushirikiana ili kiwanda
kiendelee kufanya kazi lakini pia kiendelee kutoa ajira kwa watanzania yaani
kama tutazalisha kisha wasituunge mkono tutafunga Kampuni” alisema Mkurugenzi
huyo
Kiwanda hicho cha kinamilikiwa na Mfanyabiashara maarufu Mkoani Mara Vedastus Mathayo ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa msaada Mkubwa kwa Wakazi wa Mkoa wa Mara na Mikoa Jirani kwa kutoa ajira kwa vijana walio wengi .
Kiwanda hicho cha kinamilikiwa na Mfanyabiashara maarufu Mkoani Mara Vedastus Mathayo ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa msaada Mkubwa kwa Wakazi wa Mkoa wa Mara na Mikoa Jirani kwa kutoa ajira kwa vijana walio wengi .
No comments:
Post a Comment