Waandishi wa habari wakiwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kupata taarifa ya kuwasili kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba
Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw John Tuppa akisoma taarifa kwa Waandishi wa Habari ofisini kwake
Mchakato unaendelea
TUME ya Mabadiliko ya Katiba inaanza kukusanya
maoni ya kuundwa kwa Katiba mpya Mkoani Mara Novemba 19 ikianzia wilayani Tarime
katika kata ya Bumera na Tarime Mjini.
Akiongea na Waandishi
wa Habari ofisini kwake Leo Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw John Gabriel Tuppa alisema
kuwa kufika kwa tume hiyo mkoani Mara ni fursa nzuri kwa wananchi wa mkoa wa
Mara kutoa Maoni yao.
Alisema
vyema wananchi wakahudhuria kwa wingi katika Maeneo itayokuwepo Tume hiyo na
kutoa Maoni ili kuondoa dhana ya kutoshirikishwa katika kuundwa kwa Katiba
Mpya.
“Hii ni
nafasi nzuri kwa wakazi wa Mkoa wa Mara kutoa Maoni yao ili baadaye wasije
wakasema hawajahusishwa katika kuundwa kwa Katiba Mpya” alisema mkuu huyo wa
Mkoa.
Mkuu huyo wa
Mkoa aliwaomba wananchi wa mkoa wa Mara kushirikiana vyema na Tume hiyo ili
ifanye kazi zake kwa Amani na kuondoa dhana ya kwamba Mkoa wa Mara una watu
Wakorofi.
Alisema
tayari ameishawasiliana na Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani hapa ili
kuhakikisha wananchi wanatoa Maoni yao kwa Amani na kuongeza kuwa wananchi
wanapaswa kuvumiliana katika utoaji Maoni kwani kila Mtu hutoa kile anachoona
kinafaa.
“Mimi naomba
Wananchi wa Mkoa wa Mara wawe watulivu na Wavumiliane katika kutoa Maoni maana
kila mmoja ana mtazamo wake katika kutoa Maoni” alisema Bw John Tuppa
Tume hiyo ya
Mabadiliko ya Katiba ina jumla ya watu 14 ambapo inatazamiwa kumaliza kazi ya
ukusanyaji Maoni Desemba 19 katika kata
ya Kibara wilayani Bunda.
Wakati huo
huo Mkuu huyo wa Mkoa wa Mara alisema kuwa kumekuwepo na watu kutoelewana
katika eneo la Ng’ereng’ere wilaya ya Tarime na kupelekea mtu mmoja kufariki
dunia.
Aidha mkuu
huyo wa Mkoa wa Mara amekanusha kuwepo kwa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe
kwani tukio hilo limetokana na watu kutofautiana.
“Nimesikia
taarifa eti Mapigano ya Koo Tarime yarejea jamani hii si kweli ile ni hali ya
kawaida kabisa na inaweza kutokea sehemu yoyote nchi mtu na mtu kutofautiana”
alisema Mkuu wa Mkoa Tuppa
Aliongeza
kuwa kwasasa Mkoa wa Mara kumekuwepo na Amani tofauti na kipindi kingine
chochote na hivyo kuondoa hofu inayojaribu kujengwa na baadhi ya watu
No comments:
Post a Comment