Mkuu wa mkoa wa Mara Bw John Tuppa akisoma ramani na baadhi ya maafisa wilayani Tarime
Na
Thomas Dominick,
Tarime.
MKUU wa Mkoa wa Mara John Tuppa ameuagiza uongozi wa Wilaya ya
Tarime kufyeka mazao yote yaliyomo ndani ya eneo la Serikali ili
kuondo migogoro ya aridhi ya wananchi wa kijiji cha Ng’ereng’ere na kijiji cha
Kurutamba.
Agizo hilo limetolewa jana, wakati alipokuwa katika ziara ya
kukagua eneo hilo la Serikali wilayani humo ambalo ndilo
linalosababisha machafuko ya mara kwa mara ya wananchi wa vijiji hivyo
viwili.
Tuppa alisema kuwa mazao hayo yaliyomo ndani ya shamba hilo
yamekuwa yakisababisha vijiji hivyo kupigana hasa baada ya kila mwananchi
kutakiwa kuwa katika kijiji chake kwa kuwa wananchi hao wamekuwa
wakilima shamba hilo kinyume cha sheria.
Pia ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya wilaya hiyo kuhakikisha wale wote wanaochochea
mapigano kuanzia madiwani ,wazee wa kimila pamoja na wale wote
waliohusika katika mauaji ya mwananchi mmoja hivi karibuni.
Aliwaagiza watendaji wa vijiji vyote viwili kuhakikisha
wanawajibika ipasavyo ili kuepusha migogoro ya ardhi katika eneo hilo kwa
kuonesha mipaka halali ambayo itasaidia kila mmoja kuwajibika kulingana
na ramani ya mipaka itakayokuwa imeoneshwa.
“Viongozi wa kitongoji na kata zote ni kwamba wafuate utaratibu
tuliopeana tunaomba ufanyike kwani kama ungekuwa umefanyika sisi tusingekuja
hapa matatizo hayo tote mngekuwa mmesha yatatua na sio kusubiri mpaka madhara
yatokee tumechoshwa na migogoro ya Tarime ya mara kwa mara”Alisema Tuppa.
Alisema kuwa kitu kikubwa hasa kinachowachanganya wananchi ni mipaka ya
kijiji na mipaka ya eneo lililopo ambalo ndilo linaloleta matatizo
hivyo ambaye hata ridhika afate utaratibu na sio kuchua sheria
mikononi.
Kwa Upande wa wahanga wa mapigano hayo wakazi wa kijiji cha Nyamaraga walisema
kuwa wao wanachotaka ni Serikali kuingilia kati kwa kuwasaidia kutatua
matatizo hayo kwani hata wao wamechoshwa na mapigano ya mara kwa mara na
wanachokitaka sasa ni maendeleo.
Pia wameiomba serikali kuwekeza kitu chochote katika eneo hilo ambalo ndio
chanzo cha migogoro ya mara kwa mara kwa kuwa ni eneo kubwa sana lenye hekta
193.3 na ambalo lipo wazi na lenye rutuba hivyo kufanya wananchi kulima eneo
hilo kinyume cha sheria au wapewe sehemu nyingine ili wapate sehemu ya kulima
mazao ya chakula.
“Sababu hasa inayosababisha mapigano kati ya vijiji hivi viwili ni oparesheni
ya vijiji ambayo inambidi kila mtu kuwa katika kijiji chake hii
ndio iliyosababisha matabaka ya kila koo kujitenga sasa mazao waliyokuwa
wanalina katika shamba hilo nani atayasimamia na ndio yanayoleta migogoro”alisema
Christopher Mlimi.
Waliongeza kuwa toka mwaka 1992 eneo hilo ndilo limekuwa chachu ya mapigano
baina ya koo mbalimbali katika wilaya hiyo hivyo serikali ichukue hatua za
haraka ili kunusuru vifo vanavyotokana na shamba hilo.
No comments:
Post a Comment