Wanahabari wakiwa busy katika kufanya mahojiano
Dr Safina Yuma akielezea mpango wa Serikali wa mika Mitano kusaidia akina mama
Serikali imeandaa mpango mkakati wa miaka mitano utakaowezesha kupamba na ugonjwa wa saratani
ya mlango wa kizazi ugonjwa ambao unadaiwa kusababisha vifo vingi vya akina
mama nchini.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
Dr Safina Yuma alisema hayo katika
uzinduzi wa huduma za uchunguzi wa Saratani ya Kansa ya Kizazi uliofanyika
katika ukumbi wa uwekezaji mkoani Mara.
alisema kuwa huduma hiyo itasaidia kuwagundua akina
mama mapema ili wapatiwe huduma kabla madhara hayajawa makubwa na kusababisha
kushindwa kutibika.
Dr Yumo Alisema kuwa
tatizo hilo ni kubwa hapa nchini kwa akina mama wengi ambapo wamekuwa na
tatizo hilo ambalo lina mahusiano na Hiv.
Aidha
aliongeza kuwa wizara hiyo imekuwa ikitoa miongozo kwa wadau wa afya
ambapo kwa sasa imetoa miongozo ya miaka mitano,mbali na hivyo Dr Yuma alisema
kuwa huduma hiyo tayari imeishafanyika katika mikoa ya Dar Es
Salaam,Morogoro,Iringa,Kilimanjaro,Kigoma,Ruvuma na sasa mkoani Mkoani Mara.
“Wizara yetu
imekuwa ikishirikiana vizuri na wadau mbalimbali na tumekuwa tukitoa Miongozo
nah ii itasaidia sana hasa pale wakina mama watakapokuwa wanachunguzwa mapema
kabla ya tatizo hilo kuwa kubwa” alisema Dr Yuma
Akizundua Mradi huo unaotekelezwa na shirika la Ima
World Health (IMA) yenye muunganiko wa Mashirika manne yaliyounganishwa na AIDS RELIEF,Kaimu mganga
wa mkoa wa Mara Dr Omar Gamoya alisema kuwa ni faraja kwa IMA kuchagua mkoa wa
Mara kwani kumekuwepo na ongezeko kubwa la Maambukizi ya ungonjwa wa Ukimwi
ambao una Mahusiano na Kansa ya Mlango wa kizazi kwa akina mama.
Katika uzinduzi huo uliofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji wa Mkoa wa Mara Dr Gamoya alisema mkoa wa
Mara upo pembezoni hivyo ni faraja kwa wanaMara kupata huduma hiyo.
“Tunashukuru sana hawa ndugu zetu kwa kuchagua mkoa wa Mara katika huu
mpangango maana Mkoa wetu umekuwa na maambukizi makubwa sana yanyofia asilimi
7.7 na kitaalam kansa hii inaendana na Maambuzi ya HIV” alisema Dr Gamoya.
Dr Gamoya aliongeza kuwa ni vyema wataalam hao
wakatumia taaaluma yao vizuri katika kutoa huduma kwa wananchi ambao watakuwa
wanasumbuliwa na Matatizo hayo.
Awali akimkaribisha kaimu Mganga Mkuu, Mkurugenzi wa
shirika la Kimataifa IMA ambaye pia ni mwakilishi wa Mashirika hayo manne Bw Jim Cox alisema kuwa Manisapaa ya Musoma
itakuwa ni sehemu ya Pili baada ya kuanza na huduma hiyo katika eneo la shirati
wilayani Rorya.
Alisema kuwa Tatizo hilo limekuwa likiwapa wakina
mama wengi ambapo kati ya akina mama 100 wanaopimwa akina mama saba wanakutwa
na tatizo hilo.
Mkurugenzi wa shirika la kimataifa la IMA World
Health, Jim Cox alisema kuwa shirika lake kwa kushirikiana na mashirika mengine
ya kimataifa ya Aids Relief na Catholic relief Services wameamua kufungua kituo
kwaajili ya upimaji wa ugonjwa huo katika hospitali ya serikali ya mkoa wa mara
iliyopo mjini musoma.
Pamoja na Uzinduzi huo shirika hilo pia lilitoa
vifaa vyenye Thamani ya shilingi Milioni 50 ambavyo vitasaidia katika zoezi la
huduma hiyo kwa Manispaa ya Musoma
No comments:
Post a Comment