Sunday, October 7, 2012

MGODI WAOMBWA KUTOA TAARIFA ZA FEDHA ZA MIRADI

Dinna Maningo,TARIME,

Mwenyekiti wa kijiji cha Nyamwaga Wilayani Tarime Sasi Kirigiti (CCM) ameuomba Mgodi wa  Africa Barrick Gold Mine  kutoa taarifa za gharama za fedha  zinazokuwa zimetumika kutekeleza miradi yao pindi wanapoikabidhi kwa wananchi kama njia ya kupunguza malalamiko yanayojitokeza juu ya kutotolewa kwa taarifa ya fedha katika miradi ya mgodi.


Kirigiti amesema kuwa Mgodi unapaswa kufika sehemu  kuwa wawazi kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa  za fedha zinazotumika kwenye miradi yao  kupitia maandishi nasiyo kusema kwa mdomo ili  iweze kutunzwa kama kumbukumbu na  uongozi wa Serikali ya kijiji  na kwamba siyo sahihi taarifa za fedha kutolewa ndani ya mgodi na badala yake  fedha hizo zisemwe moja kwa moja mbele ya wananchi na viongozi wa serikali ya  kijiji ili wajiridhishe.


Hayo ameyasema jana wakati Naibu Waziri wa mazingira Charles Katwanga akikabidhi kisima  cha maji kwwa wananchi wa kijiji cha Nyansangero kilichochimbwa kwa msaada wa mgodi wa North Mara ABG wakati wakiwa kwenye Ziara yao mgodini  akiwa ameongozana na Naibu Waziri wa Madini Stivin Masele na viongozi mbalimbali wa Serikali.


Mkuu wa shule ya Msingi Nyansangero Wambura  Mwita amesema kuwa msaada huo wa kisima  utawasaidia wananchi pamoja  na shule  hiyo kuondokana  na tatizo la maji  ambalo limesumbua kwa muda mlefu ambapo pia aliutaka mgodi  kutoa  taarifa ya fedha za miradi  wanapoikabidhi  kwa wananchi kwa madai kuwa mgodi ulijenga tenki la maji   shule  ya msingi Nyansangero pamoja na maasa wa madawati 91 lakini hawakuwafahamisha  wala kubainisha  gaharama zilizotumika kujenga tenki  pamoja na gahara  za kila dawati.

 MANAIBU WAZIRI WALALAMIKIWA KUKABIDHI KISIMA BILA KTAJA GHARAMA

Dinna Maningo,Tarime.

BAADHI ya  wananchi wa kijiji cha Nyansangero Kata ya Nyamwaga Wilayani Tarime wamesikitishwa na kitendo  kilichofanywa na Naibu Waziri wa mazingira Charles Kitwanga na Naibu Waziri wa madini Stiven Masele kukabidhi kisima cha maji kwa wananchi  kilichojengwa kwa msaada wa Mgodi wa Afica Barrick Gold MineABG wa Nyamongo bila kuwajulisha kiasi cha fedha zilizotumika kukamilisha ujenzi wa kisima.

Kisima  hicho kilichimbwa kwa msaada  wa mgodi na kukabindiwa jana  kwa wananchi na Naibu  Waziri wa mazingira Charles Kitwanga wakati wakiwa kwenye Ziara yao katika  mgodi wa  North Mara ABG, ambapo wananchi waliukuwepo kwenye makabidhiano walisema hawafahamu kimechimbwa na kukamilika kwa kiasi cha shilingi ngapi jambo ambalo limezua malalamiko kwa wananchi wa Nyansangero.

“Nimesikitika  kuona Waziri Kitwanga  akikabidhi kisima kwa wananchi bila  hata sisi kujua  ni kiasi gani cha pesa kimetumika katika ujenzi  wa kisima  mimi nilitarajia  kabla Waziri ajakata utepe  angeuliza mgodi fedha zilizotumika badala  yake  akaa kimya na hata Waziri Masele  naye alikaa kimya bila hata kuhoji sanjari na viongozi wa Wilaya,wanakabidhi kisima kiholela hawajasema kina urefu wa futi ngapi kwani hadi wanaotoka eneo la tukio mgodi  haukusema kiasi cha pesa kilichotumika”alisema Chacha Mwita.

Mwenyekiti wa kijiji cha Nyamwaga Wilayani Tarime Sasi Kirigiti (CCM) ameuomba Mgodi wa  Africa Barrick Gold Mine  kutoa taarifa za gharama za fedha  zinazokuwa zimetumika kutekeleza miradi yao pindi wanapoikabidhi kwa wananchi kama njia ya kupunguza malalamiko yanayojitokeza juu ya kutotolewa kwa taarifa ya fedha katika miradi ya mgodi.

“Naupongeza mgodi kwa msaada wao wa kuchimba kisima  cha maji  kitasaidia wananchi kuondokana na tatizo la maji lakini naushauri mgodi unapokabidhi miradi yao  watoe taarifa  ya moja kwa moja kwa wananchi juu ya kiasi cha pesa kilichotumika kwenye miradi yao wanapoondoka bila kusema wanazua malalamiko kwa wananchi ambao walitaka kufahamu pesa zilizotumika ,pia watoe taarifa mapema ili wananchi waalikwe kuhudhuria  kwenye miradi .”alisema Kirigiti

Kirigiti alisema kuwa Mgodi unapaswa kufika sehemu  kuwa wawazi kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa  za fedha zinazotumika kwenye miradi yao  kupitia maandishi nasiyo kusema kwa mdomo ili  iweze kutunzwa kama kumbukumbu na  uongozi wa Serikali ya kijiji  na kwamba siyo sahihi taarifa za fedha kutolewa ndani ya mgodi na badala yake  fedha hizo zisemwe moja kwa moja mbele ya wananchi na viongozi wa serikali ya  kijiji ili wajiridhishe.

Mkuu wa shule ya Msingi Nyansangero Wambura  Mwita alisema kuwa msaada huo wa kisima  utawasaidia wananchi pamoja  na shule  hiyo kuondokana  na tatizo la maji  ambalo limesumbua kwa muda mlefu ambapo pia aliutaka mgodi  kutoa  taarifa ya fedha za miradi  wanapoikabidhi  kwa wananchi kwa madai kuwa mgodi ulijenga tenki la maji   shule  ya msingi Nyansangero pamoja na maasa wa madawati 91 lakini hawakuwafahamisha  wala kubainisha  gaharama zilizotumika kujenga tenki  pamoja na gahara  za kila dawati.

No comments:

Post a Comment