Friday, October 12, 2012

HABARI KUTOKA IRINGA


WANAWAKE wanaojishusha hadhi kwa kujirahisisha katika Nyanja mbalimbali  katika jamii ikiwemo burudani biashara na katika siasa wametakiwa kuacha tabia hiyo mara moja kwa kuwa siyo desturi kwa mwanamke kujihusisha na mambo hayo kwani yanapoteza fursa na haki zao katika jamii.

Hayo yamesemwa na Ritha Mlagala makamu mwenyekiti wilaya wa halmashauri ya wilaya ya Iringa vijijini katika mdahalo wa haki na fursa sawa kwa jinsia zote uliofanyika katika kata ya Nzihi jimbo la Kalenga Iringa ulioandaliwa na mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali katika mkoa wa Iringa (ICISO-UMBRELLA).

“Ipo dhana potofu ambayo imejengeka miongoni mwa wanawake wengi kuwa wanaume ndio wenye maamuzi makubwa katika na kumpa madaraka makubwa katika kufanya maamuzi na hivyo kuwafanya wengi kukubali kutumiwa katika vitu vingi vya starehe mfano kutumiwa katika nyimbo za wasanii na katika siasa kufanya kampeni  kwa wengine huku wakiziacha nafasi hizo kwa kudhani kuwa hawana uwezo wa kuongoza”alisema Mlagala

Ameeleza kuwa ipo haja kubwa ya wanawake kusimama na kujua haki zao katika Nyanja za kimaendeleo katika jamii kama siasa. Na kusema serikali imetoa fursa nyingi sana kwa wanawake lakini wameshindwa  kuzitumia na kuwataja baadhi ya wanawake ambao wamefanikiwa katika siasa akiwemo yeye pamoja na wenye msimamo kama Dkt Asha Rose Migiro ambao wana nafasi kubwa katika siasa kwa sasa.

Pia ameongeza kuwa wanawake wengi wamekuwa hawana upendo na wamekuwa wakikatishwa tama na wanawake wenyewe kwa kudharauliana kuwa hawawezi na kuwataka wanawake kujiheshimu na kuvaa mavazi yanayositiri miili yao ili kuweza kuboresha maadili katika jamii.

Maria sanga ni mama mkazi wa kijiji cha Nzihi anakiri kuwa wanawake wengi hawajaelimika na hawajiamini na hii ni kutokana na kutokuwepo kwa elimu ya kutosha kuhusu haki zao.

“Tatizo kubwa kubwa sisi wakinamama sisi wenyewe kwa wenyewe hatuaminiani lakini kama elimu hii ya fursa na haki itaendelea kumuelimisha huyu mwanamke kweli tunaweza kuelimika mwanamke akielimika jamii nzima itaelimika”alisema sanga

Naye Abdusalani Mkata ameilaumu serikali na ngazi za juu katika unyanyasaji wa mwanamke na kueleza kuwa wanawake wengi wamekuwa wakoneshwa maungo yao katika televisheni na katika mabango ya matangazo na serikali bado inafumbia macho hali hiyo na kutoipiga marufuku na kufanya tabia hiyo kuonekana ya kawaida na kuendelezwa katika jamii.

James Ndota ameeleza kuwa amegndua wanawake wengi hawapati haki zao hii ni kutokana na wao wenyewe kutoamini kuwa fursa wanaopewa kuwa wanaweza na kutoa mfano wa vikundi mbalimbali vilivyopo katika jamii wanaposhirikishwa katika vikundi vinavyojumuisha wanaume na wanawake wengi wao hukwepa na kusema kuwa hawawezi na kuwa wamekuwa hawajiamini.

“Wito wangu ni kwamba naomba kila mmoja atambue kwamba anahaki ya kumtanguliza mwanamke kuwa anaweza katika nafasi zote na kuleta maendeleo kuanzia ngazi ya familia na katika jamii”alisema Ndota
==================================
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Mhe.Ritta kabati ametoa mifuko kumi ya saruji ,madawati na vitabu kwa shule ya msingi kibwabwa wakati wa mahafari ya shule hiyo yaliyofanyika leo katika viwanja vya shule sekondari ya hiyo kata ya kitwiru mkoani Iringa .

akizungumza na wazazi na wanafunzi wa shule hiyo katika mahafari hayo amesema kwamba wazazi wanatakiwa kuchangia zaidi katika elimu ya msingi kwa kuwa ina matatizo makubwa sana na elimu ya msingi ndio kila kitu hivyo hakuna budi wazazi wawape msingi mzuri wa elimu kuliko kuchangia zaidi katika mambo ya sherehe.

shule hiyo inakabiliwa na matazizo ya vyoo, vitabu na madawati na viwanja vya michezo na kwa kuelewa hivyo mbunge huyo wa viti maalimu  ametoa vitu hivyo kwa lengo la kujengea choo cha walimu ambako hapo mwanzo walimu wanachangia choo na wanafunzi.

aidha amewapongeza wazazi na walimu wa shule hiyo kwa juhudi kubwa wanayofanya kupandisha kiwango cha elimu katika shule hiyo kuliko ilivyokuwa mwanzo.

No comments:

Post a Comment