Teodoro Obiang
Teodoro Obiang ndiye anayeshikilia madaraka kwa muda mrefu zaidi.
Kiongozi huyo mwenye miaka 69 aliipindua serikali ya nchi yake ya Guinea
ya Ikweta mwaka 1979. Miaka 10 baadaye alichaguliwa kuwa rais wa nchi
hiyo katika uchaguzi wa kwanza huru. Obiang alichaguliwa tena katika
chaguzi za mwaka 1996, 2002 na 2009. Kipindi chake cha urais kitakwisha
mwaka 2016.
Paul Biya
Kiongozi huyu mwenye umri wa miaka 79 amekuwa akiiongoza nchi ya
Cameroon iliyoko Afrika ya Magharibi kwa karibu miaka 30 sasa. Licha ya
kuwapo kwa tuhuma ubatilishaji wa kura, alichaguliwa tena katika chaguzi
za urais za mwaka 1997 na 2004. Biya aliibadili katiba ya nchi yake
mwaka 2007 ili kupata kutawala tena. Mwaka 2011 alichaguliwa tena ingawa
upinzani ulimshutumu kwamba alibatilisha kura.
José Eduardo Dos Santos
Yeye ana umri wa miaka 69 na amekuwa akiitawala Angola tangu mwaka
1979 bila ya kuchaguliwa na wananchi. Kulingana na katiba mpya ya Angola
iliyotungwa mwaka 2010, rais hapaswi tena kuchaguliwa moja kwa moja na
wananchi. Mwenyekiti wa chama kinachopata kura nyingi katika uchaguzi
ndiye anayekuwa rais. Hivyo Dos Santos ataweza kuendelea kubaki
madarakani kihalali kwa miaka mingi zaidi.
Mswati III
Anatambulika kama mtawala pekee wa Afrika: Mswati III. Alikirithi
kiti cha kifalme kutoka kwa baba yake Sobhuza II. mnamo mwaka 1986.
Tangu wakati huo amekuwa akitawala nchi yake kwa kutoa amri huku
akikataa aina yoyote ya demokrasia. Swaziland ni miongoni mwa nchi
masikini zaidi duniani. Takriban asili mia 26 ya raia wake wameathirika
na ugonjwa wa Ukimwi.
Yoweri Museveni
Yeye aliingia madarakani mwaka 1986 kwa kutumia nguvu baada ya
kuuangusha utawala wa kidikteta Uganda na baada ya hapo kuanzisha
utawala mwingine wa aina hiyo hiyo. Kwa sababu ya kubadilishwa mara kwa
mara kwa katiba ya Uganda, Museveni sasa amekuwa akiitawala nchi hiyo
kwa miaka 26. Museveni amefuta mpaka wa muhula wa rais na hivyo aliweza
kuchaguliwa tena mwaka 2011.
Robert Mugabe
Watu wengi walikuwa na matumaini makubwa na Mugabe pale
alipochaguliwa kuwa waziri mkuu mwaka 1980 na miaka saba baadaye
kuchaguliwa kuwa rais. Lakini alianzisha utawala wa kidikteta na
kuitumbukiza nchi yake katika mzozo wa chakula na wa kifedha. Tangu
mwaka 2008, imebidi Mugambe aiongoze nchi pamoja na mpinzani wake Morgan
Tsvangirai. Hadi leo Zimbabwe inasubiri mabadiliko yaliyoahidiwa.
Blaise Compaoré
Idriss Déby
Awali, Idriss Déby Itno aliyezaliwa mwaka 1952, alikuwa mfuasi wa
kundi la waasi. Mwaka 1990, Déby alimwangusha kutoka madarakani Hissène
Habré na kuteuliwa kuwa rais wa Chad mwaka 1991. Mwaka 2004, Déby
aliibadilisha katiba ya Chad ili kubakia madarakani. Waasi walijaribu
kumwondoa madarakani mwaka 2006 na 2008 lakini bila mafanikio. Mwaka
2011 alichaguliwa kuitawala nchi yake kwa muhula wa nne.
Denis Sassou Nguesso
Nguesso aliingia madarakani mwaka 1979 lakini alishindwa katika
uchaguzi huru wa kwanza kufanyika Congo Brazaville mwaka 1992. Miaka
mitano baadaye alitoka uhamishoni na kujitwalia madaraka kwa nguvu.
Katiba ya mwaka 2002 inaeleza kwamba mgombea wa urais haruhusiwi kuwa na
umri unaozidi miaka 70. Hivyo Nguesso, mwenye umri wa miaka 69,
hataweza kugombea urais katika uchaguzi wa mwaka 2016.
Abdoulaye Wade
Abdoulaye Wade amelazimika kuachia madaraka. Katika duru ya pili ya
uchaguzi iliyofanyika Senagal tarehe 25.03.2012, mpinzani wake Macky
Sall alipata kura nyingi zaidi. Hata hivyo Wade, aliyetarajia kuiongoza
nchi yake kwa muhula mwingine, amekubali kushindwa na amempongeza Sall
kwa ushindi wake.
No comments:
Post a Comment