Sunday, June 19, 2011
UNYANYASAJI WA WATOTO CHANZO CHA KUKIMBILIA MITAANI
MUSOMA
JAMII imetakiwa kuheshimu haki za watoto na kuzithamini ikiwa pamoja na kuwasikiliza watoto kama ishara ya kuonyesha upendo na kuthamini mchango wa waototo
Hayo yamesemwa mjini hapa na wadau mbalimbali wanaotetea haki za watoto mbalimbali katika warsha ya siku tano iliyoandaliwa na shirika la kusaidia wajane na watoto (Center for widows and Children Assistance) tawi la Musoma ambayo imefanyika katika ukumbi wa angilikana mjini hapa.
Akiongea na waandishi wa habari mara baada ya warsha hiyo mjini hapa Wakili na mwanasheria Mwanadamizi wa shirika hilo Ostack Mligo tawi la Musoma alisema kuwa mradi huo wa haki za watoto ni muhimu kuieleza jamii hasa katika kipindi hiki ambacho kumeonekana jamii kukiuka haki za watoto.
Alisema warsha hiyo iliyodhaminiwa na wafadhili kutoka nchini Uholanzi ni mahususi katika jamii kutambua haki za watoto ambapo kwa mkoa wa Mara watoto wanatendewa visivyo.
“Mradi huu ni kutaka kuifahamisha jamii juu ya haki za watoto ambazo zimekuwa zikikiukwa hapa mkoani Mara”
Mwansheria huyo alisema kuwa kumekuwepo na vitendo vya kinyanyasaji kwa watoto na hasa kuwatumikisha katika migodi ya dhahabu na sehemu za uvuvi hivyo semina hiyo ni ishara nzuri kwa jamii katika kupunguza vitendo vya kinyanyasaji.
Wakili Mligo aliongeza kuwa ugomvi katika familia pia unasababisha ukosefu wa haki za watoto huku akisema kuwa jamii imetakiwa kushikamana ili kukomesha vitendo hivyo ikiwa pamoja na kutoa elimu
“Jamii lazima ishikamane katika hili na kutoa elimu ya kutosha juu ya haki za watoto hasa katika kipindi hiki tunachoadhimisha siku ya mtoto wa Afrika” aliongea wakili huyo.
Naye mwezeshaji wa warsha hiyo kutoka jijini Dar es Salaama mwanasheria Projestus Rwehumbiza alisema jamii inatakiwa kuthamini haki za watoto ikiwa pamoja na kufahamu sheria ya mtoto namba 21 ya mwaka 2009
Alisema sheria hiyo ni mpya hivyo jamii inatakiwa kuisoma na kuelewa ili baadaye wasije wakajiingiza katika matatizo baada ya kukiuka sheria hiyo.
“ Sheria hii ni mpya na kama ni mpya jamii inatakiwa kuifahamu ili isije ikajikuta inapata matatizo kwa kigezo cha kutojua sheria hiyo” alisema mwezeshaji huyo
Aidha Mkaguzi msaidizi wa jeshi la Polisi mkoani Mara Fatuma Mbwana alisemakuwa vituo vingi mkoani Mara havina mahabusu za watoto kitu ambacho kinakiuka haki za watoto.
Warsha hiyo ya siku tano ilikuwa mahususi katika kuangalia juu ya ongezeko la watoto wa mitaani ikiwa ni njia ya kukumbuka siku ya mtoto wa Afrika
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment