Saturday, September 1, 2012




WAFANYABIASHARA MUSOMA WAILALAMIKIA MANISPAA YA MUSOMA

 Augustine  Mgendi

MUSOMA

Wafanyabiashra wa Soko la Mwigobero Manispaa ya Musoma mkoani Mara wameulalamikia  uongozi wa Manispaa hiyo kutaka kuwaondoa katika Soko hilo bila kuwatengenea Maeneo Mengine ya kufanyia Biashara Zao


Wakiongea kwa Nyakati tofauti katika eneo la Soko hilo la Mwigobero,Wafanyabiashara hao walisema kuwa eneo hilo limekuwa msaada mkubwa katika kuendesha Maisha yao ya kila siku katika eneo hilo.

Walisema Uongozi wa Manispaa umeshindwa kuwaweka wazi ni wapi wataelekea baada ya kuondolewa katika eneo hilo na hivyo kuendelea kufanyabiashara bila kujua hatima yao.


  “Mpaka sasa ndugu yangu hatujui wapi tutaenda Maana naona kama hawa Manispaa wanataka kutuhatarishia Maisha yetu na Familia zetu,hapa ndipo tunapata Chakula chetu cha Kila siku halafu wanasema wanataka watutoe hapa sasa tutaenda wap”? alisema Juma Masambo mfanyabiashra katika Soko hilo

Akiongea kuhusu Malalamiko hayo Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini Vincent Nyerere alisema kuwa hakuna Mfanyabiashara yeyote atakayeondolewa katika eneo la Soko la Mwigobero bila kuonyeshwa sehemu nyingine ya kufanyia  biashara hiyo.

Akiongea kwa njia ya Simu kutoka Jijini Dar es Salaam,Mh Nyerere alisema kuwa zipo taarifa kuwa  Wafanyabiashara hao wanatakiwa kuondoka katika Eneo hilo la Soko la Mwigobero kupisha ujenzi wa soko la kisasa kwa ushirikiano na Mamlaka ya Bandari.

         Mh Nyerere katikati akitetea jambo na wabunge wenzake

Aidha aliongeza kuwa Wafanyabiashara wote waliopo katika eneo hilo hawataondoka eneo hilo bila kupewa eneo lingine,amesema Wafanyabiashara hao watapata Vibanda sehemu watakayotengewa hivyo waondoe  wasiwasi.

  ‘Yap ni kweli lakini mimi nataka kusema kuwa hao wafanyabiashra wasiwe na wasiwasi maana hakuna Mfanyabiashara atakayeondoka hapo bila kupewa eneo la kufanyia biashara” alisema Mbunge huyo

Naye Mstahiki Meya wa Manisspaa yaa Musoma Alex Kisurura akiongelea  Sakata hilo  alisema kuwa tayari Mamlaka ya Bandari imetoa fidia kwa wafanyabiashara 46  walikuwa ndani ya soko hilo wakati wa Tathimini.

Kwasababu hiyo Mstahiki Meya  alisema kuwa wananchi wa eneo hilo la Mwigobero hawapaswi kuwa na hofu katika kufanyabiashara katika eneo hilo na hivyo kuwataka wafanyebiashara zao kwa amani.

 ‘Mimi naweza kusema wafanyabiashara hao wasiwe na wasiwasi kwani lazima tuhakikishe wanapata Maeneo mengine ya kufanyia Biashara” alisema Mstahiki Meya

Eneo la soko la Mwigobero linatarajiwa kujengwa kisasa kwa mujibu wa Viongozi hao ambapo Manispaa ya Musoma itashirikiana na Mamlaka ya Bandari kufanikisha Ujenzi huo

No comments:

Post a Comment