WANAHABRI MARA WAPIGWA MSASA KUANDIKA HABARI ZA AFYA
MUSOMA
MUSOMA
MUUNGANO wa vilabu vya waandishi wa
habari nchini UTPC, umenza kutoa mafunzo maalum kuandika habari za afya kwa
waandishi wa habari katika mikoa yote nchini.
Hatua hiyo inalenga kuwajengea uwezo
waandishi wa habari kuandika habari za afya zilizofanyiwa utafiti wa kina
kwa lengo la kuboresha sekta afya na kufikisha ujumbe sahihi kwa jamii.
Mkurugenzi wa UTPC Bw Aboubakar
kassan, ameyasema mjini Musoma wakati wa mafunzo ya kwanza ya siku nne kuanza
kutolewa nchini kwa waandishi wa habari mkoani Mara ikiwa ni sehemu ya utatuzi
wa matatizo na kuibua changamoto zinazokabili utoaji wa huduma ya afya nchini.
Amesema kwa muda mrefu jamii imekuwa
ikikabiliwa na sintofahamu juu ya kujikinga na maambukizi ya magonjwa hususan
Ukimwi kutokana na waandishi nchini kutoandika habari ambazo zimefanyiwa
utafiti wa kina ambao haotoi majibu ya namna ya kujikinga na maambukizi
mapya.
Kwa sababu hiyo ametoa wito kwa
wanahabari mkoani Mara kutumia vema nafasi ya mafunzo hayo kwa lengo la kuibua
changamoto zinazokabili sekta ya afya hasa maeneo ya vijijini ili kuwezesha
wananchi kutumia mbinu bora za kujikinga na maradhi.
Kwa mujibu wa mwezeshaji wa mafunzo
hayo DK Ahmed Twaha,amesema takwimu za kiafya hususan katika maeneo ya vijijini
zinaonesha kuwa zaidi ya asilimia 60 ya wagonjwa wanaofika katika vituo vya
afya ni wanawake na watoto hivyo wanahabari wanapaswa kuibua mbinu kadhaa ya
kunusuru kundi hilo kwa kuripoti njia bora za kujikinga na maambukizi ya
maradhi kama vile Ukimwi na Malaria.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
BUNDA
Makarani 15 ambao wameshiriki katika
mafunzo ya namna ya kujaza madodoso yatakayotumika wakati wa zoezi la Sensa ya
watu na makazi wilayani Bunda mkoani Mara,wameondolewa kushiriki mafunzo
hayo baada ya kubainika kutojua kusoma wala kuandika.
Mratibu wa Sensa katika wilaya
ya Bunda Bw Donatus Wegina,amesema kuwa watu hao licha ya kupitishwa na
kamati ya sensa ya wilaya kuwa miongoni mwa makarani watakaoshiriki zoezi hilo
waliridhishwa na barua zao za maombi hivyo baada ya kubainika kuwa hawajui
kusoma na kuandika vema wameondolewa.
Amesema kabla ya kuchukua
uamuzi wa kuwaondoa watu hao,wamekuwa wakishiriki mafunzo hayo ambapo baada ya
wakufunzi wao kupitia kazi ya mshiriki mmoja mmoja ili kujua kama wanajaza
madodoso kwa kufuata maelekezo ndipo wakawabaini watu hao kujaza tofauti tena
katika mwandiko usiiosomeka kirahisi hali iliyoashiria kuwa hawajui kusoma.
Akifungua mafunzo hayo katika chuo
cha Ualimu Bunda cha mjini humo,mkuu wa wilaya Bunda Bw Joshua Mirumbe,
amesisitiza kuwa pamoja na mafunzo hayo lakini pia kutakuwepo na mchujo wa mara
kwa mara miongoni mwa washiriki ili kubaini kama kuna watu ambao hawafuati
maelekeoz katika ujazaji wa madodoso na kuwaondoa wasije wakajaza isivyo.
Jumla ya makarani 548 wakiwemo
walimu 266,watumishi wa kada mbalimbali 176 na watu wa kawaida 106 wanashiriki
katika mafunzo hayo yanayofanyikia katika vituo vya chuo cha Ualimu Bunda na
Kibara ili kuwajengea uwezo juu ya kufanya kazi hiyo vizuri siku ya sensa
Agosti 26 mwaka
huu.
,,,,,,,,,,,,,,,//,,,,,,,,,,,,,,,//,,,,,,,,,,,,,,,,//,,,,,,,,,,,,,
ABIRIA-TARIME
ABIRIA waliokuwa wakisafiri
kwenda maeneo mbalimbali Wilayani Tarime na Musoma Mkoani Mara,wameshidwa
kusafiri na kisha kuendelea kusota kituo cha mabasi mjini Tarime baada ya
wamiliki wa magari kugoma kusafirisha abiria kufuatia SUMATRA kushusha
viwango vya nauli.
Kufuatia agizo hilo la SUMATRA
polisi wilayani Tarime wamefanya zoezi la kukagua tiketi kwa abiria wote ambao
walikuwa wakisafiri kuona kama igazo hilo limetekelezwa.
Baadhi ya wamiliki wa magari katika
wilaya ya Tarime wamesema kuwa Viwango vipya vilivyopangwa na Sumatra Kutoka
Wilayani Tarime hadi Musoma ni 2900 mwendo wa km 87 ambapo kwa nauli ya
zamani ilikuwa sh 4,000, magari yatokayo Tarime kwenda Shirati ni 1,700 bei ya
zamani 5,000 km 57,magari yatokayo Tarime kwenda Nyamongo 1,700 km 37 bei ya
zamani 5,000,magari yatokayo Tarime kwenda Sirari 700 km18 bei ya zamani
ilikuwa 1,500,Tarime hadi Mugumu 5,800 bei ya zamani 7,000.
Baadhi ya wamiliki hao wa magari
wamesema kuwa viwango vya nauli vilivyopangwa na SUMATRA ni vya
chini kutokana umbali,gharama za mafuta pia havikuzingatia ubovu wa
miundombinu ya barabara katika maeneo hayo.
Kwa sababu hiyo wameitaka SUMATRA
kurekebisha viwango hivyo na kuwa mgomo huo ni endelevu hadi pale Serikali
itakaposikiliza vilio vyao nakufanya mabadiliko ya bei hiyo mpya ya nauli
kwa wasafiri.
Afisa Mfawidhi Mamlaka ya
usafirishaji Sumatra Mkoa wa Mara Bw Maico Lojasi,amesema kuwa viwango
vilivyopamgwa vimefuata taratibu zote za usafirishaji na kiuchumi na kwamba
wamiliki wa magari wamekuwa wakijipangia nauli zao wenyewe jambo ambalo
linawaumiza wananchi.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,MWISHO,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
TARIME
SERIKALI imeipatia wilaya ya Tarime
mkoani Mara vocha za pembejeo za ruzuku zeenye thamani ya shilingi bilioni
1.296 kwaajili ya ya msimu wa kilimo ambao umeishia june mwaka huu.
Afisa kilimo wa wilaya ya Tarime Bw
Bw Selvanus Gwiboha,amesema vocha hizo zimetosheleza wakulima 18,000 wakati
mahitaji yalikuwa ni wakulima 42,000 kwa wilaya ya Tarime.
Amesema pembejeo hizo ambazo
zilisambazwa kwa wakulima hao ni pamoja na mbolea ya kupandia aina ya
DAP,kukuzia aina ya UREA na Mahindi Chotara huku vijiji 89 vikinufaika na vocha
hizo za pembejeo hizo za ruzuku.
Afisa kilimo huyo ameongeza kuwa
wilaya ya Tarime ina eneo linalofaa kwa kilimo ni zaidi hekta 790,630 ambapo
eneo linalolimwa ni hekta 69,155 sawa na asilimia 76.30 eneo linalofaa kwa
kilimo.
,,,,,,,,,,,,,,,//,,,,,,,,,,,,,,,,,//,,,,,,,,,,,,,,,,//,,,,,,,
MGOMO-MUSOMA
MAASKOFU wa Kanisa la Anglikana
katika Dayosisi ya Mara na Tarime mkoani Mara,wameishauri Serikali kuacha
kutumia Mahakama na vyombo vyake vingine vya dola kama kinga katika
kumaliza migomo ya walimu,bali watumie njia ya mazungumzo katika kutatua
changamoto mbalimbali zinazowakabili walimu.
Wamesema kuwa hatua hiyo italiepusha
taifa na hatari ya kushuka kwa kiwango cha elimu kwa vile watumizi hao wanaweza
kurudi kazini na kufanya kazi kwa kinyongo na chuki kwaajili ya kuwakomoa
wanafunzi.
Kauli hiyo imetolewa mjini Musoma na
maaskofu hao Mhasham Hilkiah Omindo wa Dayosisi ya Mara na Dk Raphael Akiri wa
Dayosisi ya Tarime,wakati wakizungumza na wazazi pamoja na wanafunzi wa
shule ya ACT Mara,inayomilikiwa na kanisa hilo ikiwa ni sehemu ya kuwaaga
wanafunzi wa darasa la saba.
Wameongeza kuwa madhehebu ya dini
yamekuwa yakipata mafanikio katika sekta ya elimu kutokana na kukabiliana na
changamoto hizo kwa walimu kabla ya kuleta athari kwa jamii.
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa
shule hiyo,Bi Apaisaria Kiwori,ameonya tabia ya baadhi ya vijana ya kujiingiza
katika matendo maovu yakiwemo ya matumizi ya madawa ya kulevya jambo ambalo
amesema limechangia kwa kiasi kikubwa kudidimiza maadili ya vijana wengi
nchini.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Tarime.
WAMILIKI wa magari yanayofanya
safari zake ndani ya Wilaya ya Tarime hadi Musoma wametakiwa kustisha mgomo na
kisha kurejesha magari yao stendi ili kusafirisha Abiria vinginevyo
watakao endelea na mgomo wamedaiwa kufutiwa Leseni zao za gari.
Ni baada ya mgomo
unaoendelea wa wamiliki wa magari Tarime ambapo leo ni siku ya pili
magari Tarime kutosafirisha abiria maeneo mbalimbali ndani ya Wilaya hadi
Musoma baada ya SUMATRA Mara kushusha na kuweka viwango vipya vya
nauli kwa magari yanayofanya safari zake Tarime- Musoma,Nyamongo,Sirari,Mugumu
na Shirati,ambapo Viwango vipya vya nauli ni 2900 kutoka Tarime-Musoma,Tarime
hadi Nyamongo 1700,shirati 1700,Sirari 700 na Mugumu 5,800.
Ofisa Mfawidhi wa Mamlaka ya
usafirishaji SUMATRA Mkoa wa Mara Maico Rojas alisema kuwa endapo
wamiliki wa magari wataendelea na msimamo wao kuzuia magari watafutiwa leseni.
“viwango tulivyoweka vimefuata
taratibu zote na za kiuchumi tumefanya uchunguzi tukagundua wamiliki wa
magari wamekuwa wakijipangia nauli zaidi ya mara mbili ya viwango
vya Serikali,kuna magari madogo yanayofahamika kama michomoko hayatakiwi
kufanya kazi ya kubeba abiria isipokuwa kwa magari makubwa aina ya
Costa na Haice ndiyo yanatakiwa kubeba kwahiyo tunafanya taratibu za
kuyastisha tumefanya mabadiliko kutokana na malalamiko ya Madiwani Tarime kudai
vipunguzwe viwango vya nauli watakao kiuka tunawafutia leseni. “ alisema Rojas.
Rojas aliwataka wamiliki wa magari
wenye nia ya kusafirisha abiria kuendelea na kazi na kwamba wale wote
watakaobughuziwa na kuzuiliwa na wamiliki wenzao wanapaswa kutoa taarifa
SUMATRA au Polisi ili wawajibishwe.
Rojasi alisema kuwa kitendo cha
magari kusimama na kutofanya shughuli ni kuwakwamisha wasafi mahali waendako na
kwamba endapo wanaona bado gharama za mafuta ziko juu wanatakiwa kutoa
malalamiko yao katika mamlaka inayohusika ili hatua zichukuliwe.
Pia mmoja wa wapiga debe
stendi James Juma alisema kuwa mgomo huo wa magari umewaathiri kwani
fedha wanazozipata za kumudu familia zao zinatokana na upigaji debe wa
magari ya abiria.
Hata hivyo wamiliki wa magari
walisema kuwa bado wanaendelea na mgomo hadi pale serikali itakapofanya
marekebisho ya viwango vya nauli kwa madai kuwa hawawezi kushusha bei kwakuwa
gharama za mafuta bado ziko juu ambapo kwa upande wa disel kwa lita moja
ni 2300 huku petrol ikiuzwa 2500.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
No comments:
Post a Comment