MUSOMA.
Madiwani wa kata 17 kutoka kambi ya upinzani na baadhi kutoka
Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Halmashauri ya Musoma, wamesema kamwe
hawataunga Mkono kwa Madiwani hao kuwa chini ya Mkuu wa wilaya ya Butiama.
Wakiongea katika kikao cha Baraza la Madiwani katika
Halmashauri ya Musoma,Baadhi ya madiwani wamesema kuwa wako tayari kuwa chini
ya Mkuu wa wilaya ya Musoma na si Butiama kama baadhi ya viongozi wa
Halmashauri hiyo wanavyotaka.
Wamesema kama wataruhusu suala hilo kupitishwa
katika baadhi ya vikao,wananchi wa tarafa ya Nyanja watakuwa mbali na Makao
makuu ya wilaya hiyo na hivyo kudai kuwa ni bora wakawa karibu katika wilaya ya
Musoma.
Kuwepo kwa mvutano huo kutoka kwa madiwani wa kata 17
kati ya madiwani wa kata 34 kunafuatia
madiwani hao kudai kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw.Magina Magesa na
Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw.
Denis Ikwabe kulazima kata hizo kuwa chini ya Mkuu wa wilaya ya Butiama.
Kufuatia mzozo huo na kutoelewana ndani ya kikao
hicho Madiwani hao waliamua kutoka ndani ya Ukumbi huo na kukaa nje mpaka pale
hoja nyingine ilipoendelea.
Miongoni mwa kata kumi na saba zinazopinga kuwepo
chini ya mkuu wa Wilaya ya Butiama ni Pamoja na Kata ya
Nyegine,Etaro,Nyakatende,Mugango,Kiriba,Suguti,Nyamrandirira,Nyambono,Bugwema,Murangi,Bukima,Bulinga,Bwasi,Makojo
Bukumi,Tgeruka na Kata ya Busambara.
No comments:
Post a Comment