BABA ASKOFU
ALIASA JESHI LA POLISI TARIME.
DINNA MANINGO,Tarime
BABA Askofu
wa Kanisa la Anglicana Dayosisi ya Tarime Mwita Akili amelitaka Jeshi la Polisi
Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya kujenga mahusiano mazuri na jamii kupitia polisi
jamii ili wananchi wawe na imani na jeshi hilo.
Askofu Mwita
Akili ameyasema hayo leo katika ofisi ya Mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya wakati akikabidhi mipira 25 kwa kamanda wa
Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya Justus Kamugisha kwa ajili ya mashindano yanayoendelea
ya Polisi jamii Kata Cup 2012 katika Mkoa huo wa kipolisi
yenye lengo la kujenga uhusiano baina ya polisi na wananchi .
Askofu Akili amesema kuwa endapo jeshi la
polisi Mkoa wa kipolisi Tarime /Rorya litafanya
kazi kwa kufuata maadili pamoja
na kutenda haki ni hakika wananchi watakuwa na imani na jeshi la polisi na
kwamba kusipokuwa na mahusiano mema jeshi hilo litakosa taarifa muhimu kutoka
kwa raia hususani katika kuwafichua
waharifu
Hata hivyo
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya Justus Kamugisha amesema kuwa jeshi la
Polisi limeanzisha program za mafunzo
mara 2 kwa wiki kwa polisi lengo likiwa
kuwataka polisi kufanya kazi kwa kuzingatia maadili pamoja na kutenda haki.
No comments:
Post a Comment