NAULI MPYA YAWASOTESHA ABIRIA STENDI.
Dinna
Maningo,Tarime.
ABIRIA waliokuwa wakisafiri kwenda maeneo mbalimbali
Wilayani Tarime na Musoma Mkoani Mara wameshidwa kusafiri na kisha kuendelea kusota
stendi baada ya wamiliki wa magari kugoma kusafirisha Abiria baada ya Sumatra kushusha
viwango vya nauli ambapo polisi wanafanya zoezi la kukagua tiketi kwa abilia wanaosafiri.
Kwa mujibu wa maelezo ya wamiliki wa magari
Tarime walisema kuwa Viwango vipya vilivyopangwa na Sumatra Kutoka Wilayani
Tarime hadi Musoma ni 2900 mwendo wa km
87ambapo kwa nauli ya zamani ilikuwa sh 4,000, magari yatokayo Tarime kwenda
Shirati ni 1,700 bei ya zamani 5,000 km 57,magari yatokayo Tarime kwenda
Nyamongo 1,700 km37 bei ya zamani 5,000,magari yatokayo Tarime kwenda
Sirari 700 km18 bei ya zamani ilikuwa
1,500,Tarime hadi Mugumu 5,800 bei ya zamani 7,000.
Baadhi ya wamiliki
wa magari walisema kuwa viwango vya nauli vilivyopangwa na mamlaka ya usafirishaji
SUMATRA ni vya chini mno na nihasara
kwao kutokana na kiwango kikubwa cha mafuta kilichopo pamoja na gharama kubwa
za vifaa na matengenezo.
Hivyo
wameitaka SUMATRA kurekebisha viwango hivyo na kuwa mgomo huo ni endelevu hadi
pale Serikali itakapo sikiliza vilio vyao
nakufanya mabadiliko ya bei hiyo mpya ya nauli kwa wasafiri.
Devid Mkunyi
alisema kuwa maamuzi hayo ya viwango vipya yanajenga taswira mbaya kwa wafanya
biashara kwa madai kuwa bei iliyotolewa imepitwa na wakati kwani haiangalii
mazingira ya usafirishaji hususani barabara itokayo Tarime-Nyamongo ambayo si
ya Rami
Kutokana namugomo huo wa wamiliki wa magari baadhi ya abiria walisema kuwa kitendo cha magari kutofanya
safari zake kimewaathiri baada ya
kustisha safari kwa shuguli zao mbalimbali nakwamba mgomo huo wa wamiliki
umesababisha watu kusafiri Kutoka
Wilayani Tarime kwa usafiri wa kukodi
kwa nauli sh elfu hadi 50,00 kwenda Musoma tofauti na nauli ya zamani ya Sh
4,000,
Hata hivyo Ofisa
Mfawidhi Mamlaka ya usafirishaji Sumatra Mkoa wa Mara Maico Lojasi alisema kuwa
viwango vilivyopamgwa vimefuata talatibu zote za usafirishaji na kiuchumi na
kwamba wamiliki wa magari wamekuwa wakijipangia nauli zao wenyewe jambo ambalo
linaathiri abiria.
No comments:
Post a Comment