Tuesday, August 7, 2012

MKOA WA MARA WAPEWA TAHADHARI JUU YA UGONJWA WA EBOLA
                                      
Wananchi mkoani Mara wamepewa tahadhari juu ya Ugonjwa wa Ebola ambapo Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imepokea taarifa kutoka shirika la afya Duniani WHO kuhusu kuwepo kwa ugonjwa wa Ebola ambao umejitokeza katika nchi jirani ya Uganda.

Mratibu wa Elimu ya afya na Malaria mkoani Mara Bi. Tukae Lisso,amesema maeneo yaliyokumbwa na ugonjwa huo ni kanda ya magharibi ya nchi hiyo ya Uganda ambapo mpaka jana takriban watu 36 wamepata maambukizo na kati ya hao 19 wamepoteza maisha.

Amesema kutokana na taarifa hizo kutoka nchi jirani Wizara ya Afya na ustawi wa jamii nchini imetoa tahadhari  kwa wananchi waliopo mikoa inayopakana na nchi jirani ya Uganda kuwa Makini na ugonjwa huo.

Bi Tukae Lisso ametaja mikoa hiyo kuwa ni pamoja na mkoa wa Mara,Mwanza,Kagera,Kigoma na Rukwa ambapo wananchi katika mikoa hiyo wametakiwa kuchukua tahadhari kubwa kutokana na ugonjwa huu wa Ebola.

Amesema dalili za ugonjwa wa Ebola ni pamoja na  homa kali ya ghafla,kulegea mwili,Maumivu ya Misuli,Kuumwa Kichwa na vidonda kooni,Bi Lisso ameongeza kuwa wakti mwingine dalili hizo hufuatiwa na kutapika,kuharisha,vipele vya ngozi huku figo na in hushindwa kufanywa kazi.

Kufuatia hatua hiyo Bi Lisso amesema ugonjwa wa Ebola hauna tiba wala chanjo na hivyo amewataka wananchi mkoani Mara kuchukua tahadhari wanapomuona mtu ambaye ana dalili za ugonjwa huo wa Ebola

No comments:

Post a Comment