ALIYEKUWA MHANDISI WA BUNDA NA SASA LUDEWA AFIKISHWA MAHAKAMNI NA TAKUKURU
MUSOMA
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa Takukuru
mkoani Mara imemfikisha mahakamani aliyekuwa mhandisi wa Halmashauri ya wilaya
ya Bunda ambaye kwasasa amehamishiwa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari mkoani Mara na Naibu
mkuu wa Takukuru mkoa wa Mara Bi Yustana Chagaka ilisema kuwa Taasisi hiyo
imemfikisha Mahakamani Bw Christopher
Msafiri Nyandiga kwa kosa la kumdanganya mwajiri wake kinyume na kifungu cha 22
cha sheria ya Kuzuia na kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Alisema Bw Christopher Nyandiga kwa udanganyifu huo
ameisababishia Serikali hasara ya
shilingi milioni 24 kinyume na kifungu cha 10 ibara ya 1 pamoja na vifungu vya
57 na 60 ibara ya 1 na 2 vya sheria ya Uhujumu Uchumi namba 200 iliyorekebishwa
mwaka 2002.
Aidha Bi Chagaka alisema kuwa baada ya uchunguzi uliofanywa
na Takukuru ilibainika kuwa kampuni inayomilikiwa na Mshitakiwa iitwayo MBULLY
ENTERPRISES AND CIVIL WORKS ilipewa zabuni na halamshauri ya wilaya ya
Bunda ya kuleta Windmill aina ya POLDAW ya mita 5.8 kwa gharama ya shilingi milioni 24,kusimika
shilingi milioni 2 na kuifanyia majaribio shilingi milioni moja na hivyo
kufanya jumla ya shilingi milioni 27 kwa ajili ya mradi wa umwagiliaji Mazao katika kijiji cha Kasuguti.
Alisema mbali na hatua hiyo Takukuru pia ilibaini
kuwa Mnamo Desemba 2007 Mtuhumiwa kwa niaba ya Kampuni hiyo aliwasilisha hati
ya Malipo namba 0152 kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya Bunda zenye maelezo ya
uongo kuwa alikuwa amenunua Windmill moja aina ya POLDAW ya mita 8.2 yenye thamani ya shilingi milioni
24 huku akijua si kweli .
Naibu mkuu huyo wa Takukuru Mkoa wa Mara aliongeza
kuwa kifaa hicho hakikuwa kipya bali kilikuwa chakavu na hivyo kuisababishia
Serikali Hasara kubwa.
Aidha Bi Yustina Chagaka ametoa wito kwa Wananchi
kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa Taarifa za vitendo vyote vya rushwa.
No comments:
Post a Comment