Friday, August 10, 2012


 SERIKALI YATAKIWA KUTUMIA MIKUTANO KUHAMASISHA WANANCHI KUHESABIWA.

Dinna Maningo,Tarime

BAADHI ya wananchi Wilayani Tarime wameitaka Serikali kuwatumia viongozi wa serikali za vijiji na kata kupitia mikutano ya hadhara ili kutoa elimu ya uhamasishaji wa wananchi kuhesabiwa katika sensa na makazi.

Hayo yameelezwa kwenye kongamano  lililoandaliwa na Chama cha Democrasia na Maendeleo Chadema (CHADEMA )Kata ya Sabasaba lililofanyika ukumbi wa J.J  CLUB  leo lililowakutanisha wananchi mbalimbali mjini Tarime lililokuwa linahusu  kuhamasishaji wa wananchi kujitokeza katika  zoezi la sensa na makazi.

Wananchi wamesema kuwa licha ya Serikali kutoa matangazo,vipeperushi na kutangaza kupitia vyombo vya habari juu ya umuhimu wa sensa bado haitoshi  kutokana na kuwa wakazi wengi waishio vijijini hawafikiwi na matangazo hayo na wengine wakiwa hawana redio jambo ambalo linaweza kusababisha watu wasijitokeze kwenye sensa kutokana na kutojua umuhimu wake.

Hivyo wamewataka viongozi wa vijiji na kata kutoa elimu kupitia mikutano ya wananchi juu ya umuhimu wa mtu kuhesabiwa na kuwa kufanya hivyo itasaidia Serikali kupata idadi kubwa ya watu waliojitokeza kuhesabiwa.

Zacharia Ghati mkazi wa Ronsoti Mjini Tarime amesema kuwa uhamasishaji ni muhimu kwani unasaidia wananchi wote kuelewa umuhimu wa sensa ili waweze kutoa ushirikiano na kushiriki  katika zoezi zima la sensa

 Hata hivyo wananchi  wameiomba serikali wakati zoezi la nsensa litakapokamilika  takwimu za idadi ya watu zitumike ipasavyo na sio kutunzwa bila kufanyiwa kazi kwa madai kuwa katika sensa iliyopita haijasaidia kutokana na kuwa baadhi ya huduma za jamii zimeshindwa kuboreshwa hususani katika swala la kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora kama vile vitabu vya kutosha mashuleni jambo ambalo limeshusha taaluma kwa wanafunzi.

No comments:

Post a Comment