Tuesday, July 31, 2012

MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI AFA KWA KUCHOMWA KISU.

Dinna Maningo,Tarime

MSICHANA mmoja Angelina Masero (18) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Nyawaga,mkazi wa kijiji cha Keisangura amekufa baada ya kuchomwa kisu sehemu mbalimbali za tumbo na mwanafunzi mwenzie kutokana na sababu za wivu wa kimapenzi.

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwakwe Kamanda wa polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya Justus Kamugisha alisema kuwa tukio hilo limetokea mnamo tarehe 30 julai 2012 majira ya saa 5 asubuhi nakwamba mwanafunzi  aliyehusika na tukio hilo ni Muhono Manko (22) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule hiyo hiyo ya Sekondari Nyamwaga ambaye ni mkazi wa Nyamwaga.

“Baada ya tukio hilo marehemu alipelekwa katika  hospitali ya Wilaya ya Tarime na kulazwa bahati mbaya jana siku hiyo hiyo saa 5 usiku alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu chanzo cha tukio kinasemekana kuwa ni wavu wa kimapenzi”Alisema Kamugisha

Kamugisha alisema kuwa baada ya mtuhumiwa kutenda kosa hilo alikunywa sumu inayosadikiwa  kuwa ni dawa ya kuoshea mifugo kwa lengo la kutaka  kujiuwa na kujisalimisha kituo cha polisi Nyamwaga.
Alisema kuwa mtuhumiwa  ametibiwa katika kituo cha afya Nyamwaga na kururusiwa na kwamba yuko kituo cha polisi Nyawaga kwa mahojiano na atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

 Wakati huo huo,
MTU mmoja aitwae Sadec Stiven 17 mkazi wa Mika Wilayani Rorya Mkoani Mara amefariki dunia baada ya mwili wake kukutwa ukielea majini ziwa Victoria

Kamugisha alisema kuwa marehemu  alikwenda kwa ndugu zake waishio Bukwe kata ya Bukwe Wilayani Rorya siku ya tarehe 30 julai nakwamba marehemu  aliondoka bila kuaga  hali ambayo iliwaladhimu ndugu kumtafuta.

Kamugisha alisema kuwa  mwili wa marehemu  umepatikana leo majira ya saa 3 ukielea majini nakwamba mwili wa marehemu  umefanyiwa uchunguzi na kukabidhiwa kwa wazazi kwa mazishi.

No comments:

Post a Comment