Tuesday, July 31, 2012

MWALIMU MBALONI KWA KUDAIWA KUCHOCHEA WANAFUNZI KUANDAMANA.

Maximilliani Ngesi,Tarime

JESHI la Polisi Mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya  linamshikilia mwalimu mmoja wa shule ya Msingi Rebu Kata ya Turwa Wilayani Tarime, Ester Kasika (40) kwa mahojiano baada ya kudaiwa kuhusika kuchochea watoto kufanya maandamano baada ya kutokea kwa mgomo wa walimu hapo jana.

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya Justaus Kamugisha amesema kuwa kutokana na mgomo uliofanyika jana,  wanafunzi wa shule ya msingi Rebu waliandamana kwenda ofisi Mkuu wa Wilaya Tarime kudai haki zao za kusoma. 

                    Kamanda wa Kanda Maalum ya Tarime/Rorya Justus Kamugisha

Kamugisha amesema kuwa katika kufatilia mgomo wa walimu uliotokea jana imebainika kuwa wanafunzi wapatao 50-60 wa shule ya msingi Rebu iliyopo Mjini Tarime waliamua kufanya maandamano kuelekea ofisi ya Mkuu wa Wilaya  Tarime kwa kile walichoelezwa kuwa wanadai haki yao ya kusoma waliyoikosa kutokana na na mgomo huo wa walimu ambao unaoendelea hadi hivi sasa wilayani Hapa.

Pia  Kamugisha amewaonya  baadhi ya walimu kuwatumia watoto kudai haki zao nakuwa kitendo hicho ni kuvunja haki za watoto na kuwa Jeshi la polisi halitasita kumchukulia hatua za kisheria mtu yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo vyovyote vya kuvunja sheria za nchi.

No comments:

Post a Comment