Tuesday, January 24, 2012

MTENDAJI KATA YA MATONGO AKAMATWA

Na Dinna Maningo,Tarime

MTENDAJI wa kata ya matongo,Nyamongo Wilayani Tarime mkoani Mara BW. Deodatus Nyamuhanga Weikama amekamatwa kwa agizo la Mkuu wa  wilaya  ya Tarime John  Henjewele kwa madai kuwa mtendaji huyo amekuwa hatendei haki kwa wananchi.

 Kukamatwa kwa mtendaji huyo kumekuja baada ya malalamiko ya wananchi kudai kuporwa ardhi yao  na wanapopeleka malalamiko yao kwa mtedaji huyo hayatatuliwi badala yake  mtendaji huyo amekuwa akisaidia kupora ardhi kwa kushirikiana na watuhumiwa.

Mkuu wa Wilaya amesema kuwa kukamatwa kwa mtendaji huyo ni baada ya malalamiko ya Bi Nchagwa Kisire(36) kudai kuporwa ardhi na mme wake na kisha mme huyo  na mtendaji kufunga mji wake kwa kufuri tangu tarehe 23 na kusababisha mama na watoto kuendelea kuishi kwa kuhifadhiwa na majirani.

“Nimeagiza akamatwe ili tumuhoji kwa sababu amekuwa akilalamikiwa na wananchi kutowatendea haki hasa katika utatuzi wa migogoro ya ardhi,mfano mama huyu alilalamika kunyang’anywa ardhi na mme wake ambaye alimtelekeza mkewe Nchangwa tangu mwaka 2001 na sasa anamyanga’a makazi yake mtendaji badala ya kutatua mgogoro yeye  anashirikli kusaidia kunyang’anya ardhi!

Anaongeza’ Mtendaji aliitwa ili aje atoe majibu lakini hakufika ofisini na badala yake akapotea  akuonekana hata kazini kwa muda wa wiki mbili na baada ya kusikia tetesi karudi nilikwenda Ofisini kwake nikaagiza polisi wamkamate ili aje atueleze na sasa tumemkamata yuko hapa ofisini kwa mahojiano zaidi”anasema Henjewele.

Mtendaji huyo amedaiwa kuwa amekuwa akishindwa kutatuwa migogoro ya wananchi na badala yake amekuwa akitumia nafasi ya cheo chake kuwanyanyasa wananchi.

Hata hivyo Mwandishi wa habari hizi aliwasiliana na mlalamikaji Nchagwa kisire ambapo alidai kuwa mnamo  tarehe 23 mme wake alifika nyumbani kwakwe na kumtaka aondoke ambapo pia  mmewe na mtendaji walifunga nyumba kwa kufuri  hali ambayo imesababisha aendelee kuhifadhiwa na majirani.

Bi Kisire alisema kuwa chanzo cha mmewe kumnyang’anya eneo analoishi ni baada  ya mama huyo kutalajiwa kuhamishwa na kampuni ya mgodi wa North mara Barrick baada yakuwa eneo analoishi liko jirani na mgodi wa North Mara

 “Mme wangu alinitelekeza tangu mwaka 2001 mimi ni mke wa tatu na kila mwanamke alimpatia eneo lake la kuishi lakini baada ya eneo ninaloishi kutarajiwa kulipwa na mgodi mme kaja kapora ardhi yangu na kuniambia niondoke,nitaenda wapi na nina watoto 3chakushangaza toka anitelekeze hakuwai kunipa matumizi hata nyumba ninayoishi nimeijenga kwa nguvu zangu haki iko wapi? Ilinibidi niende ofisi ya Dc nikampelekea kilio change “anasema Nchagwa.

Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya Jastus Kamugisha alisema kuwa walimkamata mtendaji huyo baada ya kuagizwa na mkuu wa wilaya Henjewele kwa madai kuwa amekuwa atendei wananchi haki hivyo anatakiwa kwenda kuhojiwa.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,MWISHO,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

No comments:

Post a Comment