MUSOMA
Serikali
wilaya ya Musoma mkoani Mara imewataka viongozi katika ngazi
mbalimbali wilaya humo kuhakikisha inawalinda watu wenye ulemavu wa ngozi
Alibinism na kutoa taarifa haraka katika vyombo vya dola kwa wale wote wenye
njama za kufanya vitendo vya uhalifu dhidi yao.
Mkuu wa
wilaya ya Musoma mkoani Mara Bw Zeloth Stiven ametoa kauli hiyo katika shule ya
Msingi Mwisenge wakati Jumuiya ya wanachuo katika chuo cha Maendeleo ya Jamii
Buhare na Kanisa la Menonite Tanzania walipoungana na kwenda kutoa msaada wa
vitu mbalimbali yakiwemo mafuta maalum ya kutumia kujipaka.
Mkuu wa wilaya ya Musoma Bw Zelothe Steven
Alisema katika
kuhakikisha vitendo hivyo vinakomeshwa viongozi na wananchi hawana budi
kushirikiana ili kuhakikisha vitendo hivyo havitokei katika Manispaa ya Musoma.
Nao baadhi
ya wanafunzi kutoka chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare waliiomba serikali
kuhakikisha inapambana na watu wanaohusika katika Mauaji dhidi ya watu wenye
ulemavu wa ngozi katika kuhakikisha watu hao wanafikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Mmiliki wa blog hii akishow love
Rais wa Jumuiya wa chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare Bw Anania Piniel alisema kuwa kila mtu ana haki ya kuishi hivyo kuacha mauaji haya yaendeleo ni kuwanyima wengine haki ya kuishi hivyo serikali inapaswa kupambana na Mauaji haya.
"Kuishi ni haki ya kila mtu na sasa kama watu hawa wataendelea kuuawa ni kuwanyima haki ya msingi ya kuishi,tunaiomba serikali ipambane na mauaji haya" alisema Bw Anania Piniel
"Kuishi ni haki ya kila mtu na sasa kama watu hawa wataendelea kuuawa ni kuwanyima haki ya msingi ya kuishi,tunaiomba serikali ipambane na mauaji haya" alisema Bw Anania Piniel
No comments:
Post a Comment