Wednesday, July 2, 2014

POLISI TABORA YANASA MAJAMBAZI WATANO NA BUNDUKI MOJA ,JAMBAZI MMOJA AUAWA KWA KUPIGWA NA WANANCHI.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Suzan Kaganda akiwaonesha waandishi wa habari silaha aina ya SMG iliyokamatwa ikiwa na risasi mbili pamoja na watuhumiwa watano ambapo mmoja kati ya watuhumiwa hao aliyefahamika kwa jina moja la Rajab anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 30-36 alifariki dunia baada ya kushambuliwa na wananchi huko katika kijiji cha Tura wilayani Uyui. Aidha majambazi hayo yalikamatwa baada ya kufanya tukio la unyang'anyi wa kutumia silaha ambapo yalifanikiwa kupora zaidi ya shilingi milioni mbili na laki tatu na ndipo makachero wa Jeshi la Polisi kwa ushirikiano mkubwa kutoka kwa wananchi walifanikiwa kuyakamata yakiwa na silaha hiyo ambayo imedaiwa ilitumika katika tukio la uporaji pamoja na Pikipiki mbili aina ya Sanlg
Kamanda Suzan akionesha magunia  mawili na nusu ya bhangi yaliyopatikana katika msako mkali wa Jeshi la Polisi huko eneo la Wilaya ya Nzega ambapo watu watatu wanashikiliwa kuhusiana na tukio la kuwa wauzaji na watumiaji wa bhangi.


No comments:

Post a Comment