Na Mwandishi
wetu
Timu ya soka
ya Biashara United ya mjini Musoma Mkoani Mara inayojiandaa ya mchezo wa
kirafiki dhidi ya timu ya soka ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
mwishoni mwa wiki imewabamizia Timu ya Polisi Veteran ya Mjini Musoma mabao 2-0
katika mchezo wa kirafiki uliofanyika katika uwanja wa Kumbukumbu ya Karume
mjini hapa.
Mchezo huo
ambao ulikuwa na kila aina ya ufundi kutoka kwa wachezaji wa timu zote kipindi
cha kwanza kilimalizika baada ya timu hizo kutosha nguvu ya 0-0
Katika
kipindi cha Pili timu hiyo inayoongozwa na Kocha Mchezaji Aman Richard ilifanya
mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji ambapo katika safu ya ushambuliaji aliingia
Augustine Mgendi mabadiliko ambayo yaliinufaisha timu hiyo ya Biashara United
baada ya mchezaji huyo kuifungia timu hiyo mabao hayo mawili.
Akiongea
baada ya mchezo huo,Kocha huyo alisema kuwa bado timu hiyo inahitaji kufanya
maboresho kabla ya mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Bunge Mjini Dodoma.
“Tumeshinda mchezo wetu lakini bado tuna kazi
kubwa maana tunapata nafasi nyingi lakini hatuzitumii ipasavyo,sasa kwa mchezo
uliopo mbele yetu lazima tubadilike” alisema Kocha Aman
Katika
mchezo huo ambao ulishuhudiwa na baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Musoma mkoani
hapa ni maandalizi ya mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Bunge utakaofanyika
mwanzoni mwa mwezi August mjini Dodoma.
No comments:
Post a Comment