Sunday, July 13, 2014

Wananchi Butiama waua Majambazi 3 kwa kuwachoma moto


 WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wameuwawa kwa kushambuliwa na siraha za jadi ikiwemo rungu,mapanga na mawe baada ya kudaiwa kufanya uhalifu wa kuwateka wavuvi ndani ya ziwa Victoria na kuwanyang’anya vifaa vyao vya uvuvi.
Akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake,kamanda wa jeshi la polisi mkoani Mara Philip Karangi alisema tukio hilo lilitokea julai 9 majira ya saa 5 usiku katika kisiwa cha Iriga kilichopo Kijiji cha Busamba Kata ya Etaro Wilaya ya Butiama.

No comments:

Post a Comment