Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani za Uchaguzi ya
TFF, Julius Lugaziya (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar
es Salaam kuhusu uamuzi wa kamati hiyo kumrudisha mgombea wa Rais katika klabu
ya Simba, Michael Wambura. Kulia Mkurugenzi Msaidizi Sheria na Wanachama TFF,
Eliud Mvella.(Picha na Francis Dande)
Baadhi ya mashabiki wanaomuunga mkono mgombea wa
nafasi ya Rais wa klabu ya Simba, Michael Wambura wakishangilia nje ya ofisi za
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), baada ya kamati ya Rufaa ya TFF, kumrejesha
katika kinyang’anyiro hicho.Picha na Francis Dande
--
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetupilia mbali
pingamizi lililowekwa na wanachama wa Simba na kumruhusu mgombea wa
nafasi ya urais katika klabu hiyo, Michael Wambura kuendelea na mchakato
huo.
Mwenyikiti wa Kamati ya Rufaa wa TFF, Julius Lugazia alipotangaza
rufaa hiyo alisema Wambura ni mwanachama halali wa Klabu ya Simba
kisheria hivyo anayo haki ya kugombea nafasi hiyo kama wagombea wengine
kwani amekuwa akishirikishwa katika kamati mbalimbali huku mchango wake
wa kimawazo ukitumika ndani ya klabu hiyo
Mashabiki wa Klabu ya Simba ambao ni wafuasi wa Wambura, walipokea
taarifa hiyo ya TFF kwa mikono miwili na kushangilia kwa staili ya
kipekee kwenye makao makuu ya klabu hiyo mtaa wa Msimbazi kwa
kufurahishwa na maamuzi hayo.
(Picha na Stori Deogratius Mongela GPL)
No comments:
Post a Comment