Shadrack Joseph Mnemba (MBETA)
Na : Mwandishi wenu
Mnemba
ni msanii wa filamu aliyezaliwa huko mkoani Dodoma miaka kadhaa
iliyopita,katika harakati zake za kutafuta maisha, msanii huyu alihamia
mkoani dar es salaam huku lengo lake kuu likiwa ni kuja kuungana na
wasanii wengine wa fani hii ili aielewe na kujifunza na kuwa nyota wa
filamu Tanzania. Haikuwa rahisi sana kama alivyokuwa anawaza kwani
alikutana na changamoto nyingi zilizomfanya kutofanikiwa kwa haraka na
kumfanya kuwa mmoja kati ya wale wengi wanaohangaikia kufahamika katika
sanaa hii.
"Nilikuja Dar es salaam nikiwa na lengo moja la kuwa mmoja
kati ya mastaa wa sanaa hii lakini nilikutana na changamoto nyingi
ambazo mbali na kunijenga kiakili pia zimenifanya kuzidisha zaidi juhudi
za kutaka kufika mahali ambapo nataka kufika, nilisha wahi kupita
katika vikundi mbali mbali vya sanaa na nilifanya mazoezi mengi ya sanaa
japo mpaka sasa sijatoka lakini naamini kuna siku nitasimama mwenyewe
na ntafanikiwa kuwa mmoja wa wasanii bora wa sanaa hii ya uigizaji" alisema msanii huyo.
Hapo juu ndiyo kava la filamu ya kwanza ambayo ameiigiza akiwa mmiliki inayokwenda kwa jina la
"MSUKULE HAI"
Hata hivo kwa mtazamo mpana Mtandao wako imejibainisha kuwa Shadrack (Mbeta) ni msanii ambaye anahitaji sana msaada wako wa kumsapoti kwenye kazi zake za sanaa kama anavobainisha mwenyewe hapa."Chamsingi naomba sana watanzania waniunge mkono katika kazi zangu za sanaa, pia naomba waniunge mkono pale filamu yangu ya MSUKULE HAI itakapoingia sokoni kwa kuinunua kwa wingi ili harakati zangu zizidi kusonga mbele na ndoto zangu za kuvuka kimataifa zitimie".
Hata
hivo msanii huyu aliutanabaisha Mtandao wako ya kuwa katika harakati
zake za kusaka ridhiki hajaishia tu kucheza filamu pia anaweza, kuimba Muziki na kucheza Ngoma za kitamaduuni pamoja na kufanya maonesho ya Kula moto,
kwa wasanii mbali mbali ambao watapenda kumshirikisha katika kazi zao
au kujua zaidi kazi zake, mtaweza kumpata kwa mawasiliano ya namba hizo
hapo chini. nk.
+255 713 254553
+255 767 254553
Email: mbetasm@gmail.com
No comments:
Post a Comment