Waandishi wa habari mkoani Mara wakiwa katika mkutano na Katibu tawala Mkoa wa Mara
Katibu Tawala wa mkoa wa Mara Benedict Ole Kuyan ametoa
ratiba ya awali ya shughuli nzima ya kuuga mwili wa marehemu John Tupa
na kuwashukuru Waandishi wa Habari kutokana na kutumia nafasi yao
kuwajulisha watanzania juu ya taarifa ya kifo cha mkuu wa mkoa wa Mara.
Amesema
shughuli ya kutoa salamu za rambirambi pamoja na kuuaga mwili wa
marehemu itaanza saa 1;00 hadi saa 3;20 katika makazi ya mkuu wa mkoa na
baadae kupelekwa Kanisa Kuu Parokia ya Musoma Mjini saa 3;20 hadi saa
5;00 kwa ajili ya ibada na kisha kuondoka kuelekea uwanja wa ndege wa
Mwanza kwa ajili sa safari ya kuelekea Kilosa mkoni Morogoro kwa
shughuli ya mazishi kwa kupitia mkoani Dodoma.
No comments:
Post a Comment