Serikali
Mkoani Mara imezitaka halmashauri za wilaya mkoani humo kukusanya Mapato na
kisha sehemu ya Mapato hayo kutumika katika kupambana na Vitendo vya Uvuvi
haramu vinavyofanyika ndani ya Ziwa Victoria.
Mkuu wa
Mkoa wa Mara Bw John Gabriel Tuppa alisema hayo wakati wa kuteketeza zana
haramu zaidi elfu moja zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia tatu
kufuatia Operesheni za doria zilizoendeshwa na kikosi cha doria,Maafisa
Uvuvi,Polisi na BMU mkoani hapa.
Bw Tupa ambaye
alichoma zana hizo haramu amesema Uvuvi huo utakwisha kama kutakuwa na
Ushirikiano kuanzia kwa Wanasiasa na kufanya ukaguzi wa Mara kwa Mara ndani ya
ziwa Victoria na Maduka yanayouza zana hizo.
Kwa upande wake afisa Mfawidhi
Msimamizi na Ulinzi wa Rasilimali za Uvuvi mkoani Mara Bw Braison Gasper Meela
alisema zana hizo haramu zinateketezwa kwa Mujibu wa Kanuni ya Uvuvi ya Mwaka
2009 ambayo inapiga Marufuku Kutengeneza,kuhodhi,kuuza au kumiliki na kutumia
Zana hizo katika shughuli za Uvuvi ndani ya Ziwa Victoria.
Zana hizo
haramu ambazo zimeteketezwa ni pamoja na
Kokoro 652,Nyavu utali 4084,Nyavu za tupatupa 40,Nyavu za Makila 8774,Kamba za
Kokoro 53020 na vyavu za Dagaa 28.
Matukio katika Picha
Bw John Gabriel Tuppa
No comments:
Post a Comment