TARIME
Watanzania
wametakiwa kuheshimiana na kuvumilia ili Mawazo yanayotolewa katika
Jamii yatumike kuleta Maendeleo kiroho na Kimwili katika sehemu mbalimbali hapa
nchini na Taifa kwa ujumla
Hayo
yameelezwa na Mke wa hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere,Mama
Maria Nyerere wakati akihutubia wananchi wa kijiji cha Nyamwaga wilaya ya
Tarime Mkoani Mara katika uzinduzi wa Shule ya Sekondari ya Julius Kambarage
Nyerere iliyojengwa na Mgodi wa African Barrick North Mara.
Mama Maria alisema kuwa kila jambo linahitaji uvumilivu na kuheshimu mawazo ya kila mmoja ili kujenga umoja na Mshikamano katika Jamii.
Mjane wa Baba wa Taifa mama Maria nyerere kulia
Awali
akimkaribisha Mama Maria Nyerere,Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw John Gabriel Tuppa
ameshauri kujengwa Makumbusho ndogo katika taasisi mbalimbali ambazo zinapewa
jina Mwalimu Nyerere huku Meneja wa Mgodi wa North Mara Bw Gary Chapman alisema kuwa ujenzi wa shule hiyo umegharimuaidi ya shilingi Bilioni mbili huku akisema kuwa Mgodi huo utaendelea kuimarisha na kutekeleza Miradi mbalimbali katika maeneo hayo ya Mgodi.
Katika
hatua nyingne Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Nyamwaga wameelezea kufurahiswa
na utekelezaji wa Miradi hiyo inayofanywa na Mgodi wa African Barrick North
Mara na kusema hayo hayo ndiyo Matunda ya Ushirikiano huku wakisifu jitihada za Serikali kuleta wawekezaji ambao wamekuwa na tija kwa Jamii
HABARI KATIKA PICHA
No comments:
Post a Comment