ZANZIBAR
JUMAMOSI JANUARY 18, 2014. Jeshi la Polisi Zanzibar linamshikilia
Askari mmoja wa Chuo cha Mafunzo sawa na Magereza kwa Tanzania Bara
Sajin Meja (S/Sgt) Hassan Iddi Hassan (45), kwa tuhuma za wizi wa
shilingi 1,635,000 alizoziiba kutaka katika duka moja lililopo eneo la
Makadara mjini Zanzibar.
Afisa Habari Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar Inspekta Mohammed Mhina,
amesema
tukio hilo limetokea jana majira ya saa 11.00 jioni wakati Askari huyo
akiwa amevaa kiraia, alipofika katika dukani kama mteja wa kawaida
huku muuzaji wa duka hilo akiwahudumia wateja wingine na ndipo
alipoingia ndani na kufungua droo ya pesa na kuiba kiasi cha shilingi
1,635,000 na kuanza kutimua mbio.
Inspekta
Mhina, amesema hata hivyo askari huyo alitiwa nguvuni na Polisi baada
ya kufukuzwa na wananchi na kukutwa akiwa na fedha zote alizoiba na kuokiolewa.
Naye
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar ACP Mkadam Khamisi
Mkadamu, amesema kuwa fedha zote zilizoibwa na kupatikana mikononi mwa
Askari huyo zimehifadhiwa Polisi ikiwa ni kielelezo mahakamani.
Hilo
ni tukio la tatu kutokea mjini Zanzibar katika kipindi cha mwaka huu
ambapo tukio la kwanza ni lile la jaribio la wizi katika maghala ya
Bakheresa eneo la Fuoni nje kigodo ya mji wa Zanzibar ambapo watuhumiwa
watatu walikamatwa wakiwa na silaha aina ya gobore linalotumia risasi za
short gun.
Na
tukio linguine ni la kukamtwa kwa majambazi wanne akiwemo Afisa wa
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini wakiwa na silaha tatu
zikiwemo bastola mbili na SMG moja
baada ya kumvamia mfanyabiashara mmoja na kumpora milioni 11.5 eneo la
Rahaleo mjini Zanzibar.
Matukio
hayo yote yakiwa na jumla ya watuhumiwa wanane na silaha nne yaliweza
kukabiliwa kwa haraka na Polisi kufuatia msaada wa wananchi wa kutoa
taarifa za haraka polisi na wenyewe kujitolea kusaidiana na Polisi
kuwakabili watuhumiwa na kufanikisha ukamataji salama.
No comments:
Post a Comment