Sunday, January 19, 2014

Askari Magereza ashikiliwa na Jeshi la Polisi Zanzibar kwa wizi

ZANZIBAR JUMAMOSI JANUARY 18, 2014. Jeshi la Polisi Zanzibar linamshikilia Askari mmoja wa Chuo cha Mafunzo sawa na Magereza kwa Tanzania Bara Sajin Meja (S/Sgt) Hassan Iddi Hassan (45), kwa tuhuma za wizi wa shilingi 1,635,000 alizoziiba kutaka katika duka moja lililopo eneo la Makadara mjini Zanzibar.
 
 
 
Afisa Habari Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar Inspekta Mohammed Mhina,
amesema tukio hilo limetokea jana majira ya saa 11.00 jioni wakati  Askari huyo akiwa amevaa kiraia, alipofika katika dukani kama mteja wa kawaida huku  muuzaji wa duka hilo akiwahudumia wateja wingine na ndipo alipoingia ndani na kufungua droo ya pesa na kuiba kiasi cha shilingi 1,635,000 na kuanza kutimua mbio.
 
Inspekta Mhina, amesema hata hivyo askari huyo alitiwa nguvuni na Polisi baada ya kufukuzwa na wananchi na kukutwa akiwa na fedha  zote alizoiba na kuokiolewa.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar ACP Mkadam Khamisi Mkadamu, amesema kuwa fedha zote zilizoibwa na kupatikana mikononi mwa Askari huyo zimehifadhiwa Polisi ikiwa ni kielelezo mahakamani.
 
Hilo ni tukio la tatu kutokea mjini Zanzibar katika kipindi cha mwaka huu ambapo tukio la kwanza ni lile la jaribio la wizi katika maghala ya Bakheresa eneo la Fuoni nje kigodo ya mji wa Zanzibar ambapo watuhumiwa watatu walikamatwa wakiwa na silaha aina ya gobore linalotumia risasi za short gun.
 
Na tukio linguine ni la kukamtwa kwa majambazi wanne akiwemo Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini wakiwa na silaha tatu zikiwemo bastola mbili na SMG moja baada ya kumvamia mfanyabiashara mmoja na kumpora milioni 11.5 eneo la Rahaleo mjini Zanzibar.
 
Matukio hayo yote yakiwa na jumla ya watuhumiwa wanane na silaha nne yaliweza kukabiliwa kwa haraka na Polisi kufuatia msaada wa wananchi wa kutoa taarifa za haraka polisi na wenyewe kujitolea kusaidiana na Polisi kuwakabili watuhumiwa na kufanikisha ukamataji salama.
 

No comments:

Post a Comment