BUTIAMA
Zaidi ya
tani elfu nane za Chakula zinahitajika katika wilaya ya Butiama mkoani Mara ili kukabiliana na tatizo
la njaa kali ambalo limeikumba wilaya hiyo na Wananchi kushindwa kufanya
shughuli za Maendeleo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Butiama mkoani Mara Bw Josephat Maganga
ameelezea upungufu wa Chakula ulipo katika halimashauri hiyo katika kikao cha
bajeti cha barza la Madiwani na kusema kuwa tayari halmashauri hiyo hiyo
imepeleka ombi maalum katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Amesema
baada ya Tathimini iliyofanywa na halmashauri hiyo imebaini kuwepo kwa tatizo
kuwa la njaa ambapo tani 8554.5 za Chakula
zinahitajika katika kukabiliana na tatizo hilo la njaa katika halmashauri hiyo
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa halamshauri ya wilaya ya Butiama BW Magina Magesa amesema
kutokea kwa tatizo la njaa katika halmashauri hiyo lisionyeshe kuwa wananchi wa
Maeneo hayo ni wavivu katika suala la Kilimo bali ni kutokana na ugonjwa wa
Mihogo ulioikumba halmashauri hiyo
katika
Mwaka ujao wa fedha halmashauri hiyo imeeleza kupeleka Tamisemi na hazina
Maombi maalum ya Miradi Mikubwa ambayo ni ujenzi wa jengo la Utawala katika
hospital ya Butiama,Ujenzi wa Nyumba ya Mkurugenzi, ununuzi wa Magari
Manne,Ujenzi wa barabara ya kilomita 14na ujenzi wa Jengo la Utawala katika
Hamashauri hiyo ambapo miradi hiyo
itagharimu kiasi cha shilingi billion 6.7
No comments:
Post a Comment