Saturday, January 4, 2014

Mabalozi wa nyumba 10 Manispaa ya Musoma waiomba Serikali kuwakumbuka

MUSOMA
Mabalozi wa nyumba kumi katika Manispaa ya Musoma mkoani Mara wameiomba serikali kuwakumbuka na kuweka utaratibu maalum wa kuwatambua kutokana na kuwa karibu na Jamii na hivyo kusaidia katika suala la ulinzi na Usalama katika maeneo yao.

Hayo yameelezwa katika kikao ya siku moja ya mabalozi 600 kutoka Mitaa 57 ya halmashauri ya Manispaa ya Musoma mkoani Mara ambapo kikao hicho kilikuwa na lengo la kutathimini Changamoto zinazowakabili Mabalozi likiwemo suala la ulinzi na Usalama katika maeneo yao.
                  Bi Agnes Methew akiongea na Mabalozi wa Manispaa ya Musoma 


Wakiongea katika Warsha hiyo baadhi ya Mabalozi walipata nafasi ya kuongea wamesema kumekuwepo na lawama kutoka nyumba wanazoziongoza kutokana na  ahadi hewa zinazotolewa na baadhi ya viongozi,wengine wakisema kwasasa wamebaki kuwa mabalozi wa kutangaza msiba huku wengine wakiongeza kuwa mabalozi wamebaki kama punda.
"Sisi ndiyo tuko karibu sana na wananchi kama ni wau wabaya tunawajua sisi lakini hatupewi thamani mpaka wakati wa uchaguzi unapofika" alisema Bi Sofia
Kwa Upande wake Mjumbe wa UWT Taifa kutoka mkoani Mara Bi Agnes Methew amewataka Mabalozi kuvunja Makundi ambayo yamekuwa yakikigharimu chama cha Mapinduzi nyakati za Uchaguzi na kuiomba Serikali kuwataza mabalozi na kuwatambua  kama kiungo muhimu.
 "Kabla ya wote ebu tuache kwanza Makundi ambayo si mazuri ndani ya Chama lakini pia tunamuomba Rais Kikwete awatazame maana anatambua umuhimu wenu" alisema Bi Agnes
        PICHA MBALIMBALI ZA MABALOZI KATIKA KIKAO HICHO

No comments:

Post a Comment